Mke wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Asha Bilal, akiwasili kwenye Ukumbi wa VIP wa Diamond Jubilee, jijini Dar es Salaam jana jioni kwa ajili ya kuhudhuria sherehe za maadhimisho ya miaka 10 ya Taasisi ya Maznat, kama Mgeni rasmi sambamba ya kuzindua Shule ya Taasisi hiyo inayofundisha masuala ya urembo.
Mke wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Asha Bilal, akishiriki kukata Keki na Maza Sinare, ambaye ni mmiliki wa Saluni ya Maznat, ikiwa ni sehemu ya sherehe za maadhimisho ya miaka 10 ya Taasisi ya Maznat, iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Diamond jijini Dar es Salaam, jana Mei 5, 2013, sambamba na sherehe hizo pia Mama Asha, alizindua rasmi shule ya masuala ya Urembo inayosimamiwa na Taasisi hiyo.
Mke wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Asha Bilal, akihutubia wakati wa sherehe za maadhimisho ya miaka 10 ya Taasisi ya Maznat, iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Diamond jijini Dar es Salaam, jana, sambamba na sherehe hizo pia Mama Asha, alizindua rasmi shule ya masuala ya Urembo inayosimamiwa na Taasisi hiyo.
Mama Asha, akipongezwa na wageni waalikwa baada ya kusoma hotuba yake ukumbini hapo.
Sehemu ya wageni waalikwa waliohudhuria sherehe hizo.
Mmiliki wa Saluni na Taasisi ya Maznat, Maza Sinare, akiwalisha keki baadhi ya wageni waalikwa wakati wa sherehe za maadhimisho ya miaka 10 ya Taasisi ya Maznat, iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Diamond jijini Dar es Salaam jana, sambamba na sherehe hizo pia Mgeni rasmi mke wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Asha, alizindua rasmi shule ya masuala ya Urembo inayosimamiwa na Taasisi hiyo.
Mke wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Asha Bilal (kulia) akikata utepe kuashiria kuzindua rasmi shule ya masuala ya Urembo, wakati wa sherehe za maadhimisho ya miaka 10 ya Taasisi ya Maznat, iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Diamond jijini Dar es Salaam, jana. Shule hiyo inasimamiwa na Taasisi hiyo.luni na Taasisi hiyo ya Maznat, Maza Sinare. Kwa matukio ya picha zaidi bofya hapo chini.
Msanii wa muziki wa Taarab, Mzee Yusuph, akiimba jukwaani kutoa burudani wakati wa sherehe hizo.
Mama Asha Bilal, akiwaongoza wanawake waliohudhuria sherehe hizo katika kucheza muziki wa taarab, burudani iliyokuwa ikitolewa ukumbini hapo na Mzee Yusuph.
Msanii wa muziki wa Injili, Bahati Bukuku, akiimba jukwaani kutoa burudani wakati wa maadhimisho hayo.
Baadhi ya wadau wa Maznat, waliohudhuria sherehe hizo, wakisebeneka na miondoko ya taarab, ukumbini hapo.
Baadhi ya wadau wa Maznat, waliohudhuria sherehe hizo, wakisebeneka na miondoko ya taarab, ukumbini hapo.
Baadhi ya wadau wa Taasisi ya Maznat, wakihesabu fedha zilizopatikana baada ya kuchangwa na washirika wa karibu wa Taasisi hiyo ukumbini hapo jana wakati wa sherehe hizo kwa ajili ya kusaidia mfuko wa kusaidia Watoto Yatima ulio chini ya Taasisi hiyo, ambapo zilipatikana jumla ya sh. milioni 22.
Mmiliki wa mtandao wa Mafoto Jr, Nasma Mafoto (kushoto) akiwa na wadau waliohudhuria sherehe hizo.
Wasanii wa kundi la The Voice, wakitoa burudani ya kuimba 'Akapera' jukwaani wakati wa sherehe hizo.
Mabaunsa wakifungua na kuripua Shampeni kwa pamoja ikiwa ni sehemu ya kusherehesha ukumbini hapo.
Maznat, akipozi kwa picha na wafanyakazi wake...
Mama Asha Bilal, akiwaongoza wageni waalikwa kugonganisha glasi wakati wa sherehe hizo.
Kwa amani na furaha ya kutimiza miaka 10 ya Taasisi ya Maznat, wageni waalikwa waligonganisha glasi zao.
Cheeeeeeeeaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaazzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzz!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
HOTUBA YA MHE. MAMA
ASHA BILAL, KWENYE MAADHIMISHO YA MIAKA KUMI YA KAMPUNI YA MAZNAT. TAREHE
05 MEI, 2013, UKUMBI WA DIAMOND JUBILEE DAR ES SALAAM.
Waheshimiwa Mabalozi,
Mheshimiwa Naibu Waziri
wa Katiba na Sheria,
Waheshimiwa Wabunge,
Mheshimiwa Mkuu wa
Wilaya ya Temeke,
Mwenyekiti wa Taasisi
ya Sekta Binafsi Tanzania,
Viongozi wote wa
Taasisi mbali mbali nchini,
Wageni waalikwa
Mabibi na Mabwana.
Kwanza kabisa, namshukuru Mwenyezi Mungu, mwingi wa Rehema
kwa kutujaalia uzima na afya tukaweza kujumuika pamoja katika hafla hii. Pili, naomba kutoa shukrani zangu binafsi kwa
heshima niliyopewa kuwa Mgeni Rasmi, katika hafla hii ya kuadhimisha miaka kumi
ya kampuni ya Maznat Bridal Care.
Nimefarijika sana kujumuika nanyi leo katika hafla inayotupa fursa nzuri
sisi kama wanawake kujadili mambo mbalimbali yanayotugusa, kusherehekea
mafanikio aliyopata Maznat na sisi sote, kufahamiana na kufurahi pamoja.
Natoa pongezi zangu kwa wanawake wote
mliohudhuria leo, kwani mmejitokeza kwa wingi kutoka katika sekta mbalimbali za
biashara.
Mchango wa mwanamke katika familia na jamii yetu huchukuliwa
kama jambo la kawaida, bila kuchanganua majukumu mazito aliyo nayo kila siku ya
kulea watoto, kuzalisha mali, kukuza kipato, kuongeza nafasi za ajira, na
shughuli nyengine nyingi.
Licha ya kuwa
mwanamke ndiye nguzo kubwa ya nguvu kazi kifamilia na katika ngazi nyengine, lakini
bado wanawake ndiyo wanaongoza kwa umasikini.
Ni wazi kuwa ujira kwa wanawake haulingani na mchango wetu
kiuchumi. Hata hivyo, wakati umefika wa
sisi wanawake kufanya shughuli zenye kipato ili kufidia, angalau kwa kiasi cha
juhudi zetu.
Kwa maana nyengine
tuhakikishe sisi tunajilipa ujira kwa kazi zetu.
Kutokana na hilo, nichukue nafasi hii kumpongeza Bi. Mazna
Sinare kwa ubunifu wake katika sekta ya urembo, na kuendeleza kasi ya maendeleo
ya sekta hii muhimu katika uchumi wetu licha ya changamoto mbalimbali
alizokuwanazo kama mama wa familia, na mwanamke katika jamii.
Nimevutiwa sana na juhudi kubwa alizozifanya
mpaka kufikisha miaka kumi ya huduma anazozitoa, na vile vile kufanikiwa
kuanzisha mafunzo ambayo yataendeleza utaalamu wa sekta hii muhimu.
Nakupongeza sana kwa kazi kubwa kwani wahenga
wanasema “ukiona vyaelea ujue vimeundwa”.
Aidha nakuombea kwa Mwenyezi Mungu muweza wa yote azidi kukubariki na
akuzidishie mafanikio mema.
Amin.
Hafla hii ya leo ni kiungo muhimu katika kutafsiri kwa
vitendo Maazimio ya Beijing, pamoja na Malengo na Dira ya Maendeleo ya Taifa
(Tanzania Development Vision 2025) na mikakati mbalimbali ya kitaifa ya kuondoa
umasikini.
Ustadi wa kupanga shughuli
hii kwa kuweka nafasi kwenye ratiba, kusikia mafanikio ya wanawake wenzetu
katika ujarisiamali, maonesho ya bidhaa mbalimbali na kupata elimu ya huduma za
kifedha umenifurahisha sana, kwani sote tutapata elimu zaidi katika
kujiendeleza kwenye shughuli zetu za kijasiriamali.
Katika kutekeleza malengo na majukumu yeke, na ili kufikia
miaka kumi hii leo, Mazna amepitia changamoto mbalimbali ambazo zingeweza
kumfanya akate tamaa katika biashara yake.
Moja ya changamoto kubwa ni hali duni ya kiuchumi miongoni mwa wanawake
wajasiriamali, changamoto ambayo wanawake wengi wajasiriamali mnayo hapa
nchini.
Hata hivyo, Maznat ametuonesha
mfano mzuri kwa kuwa ameweza kumudu changamoto hii, kwa kutumia vizuri fursa
zinazotolewa na taasisi za kifedha hapa nchini.
Natoa wito kwa wanawake wenzangu kujifunza kutoka kwa wajasiriamali
wenzetu kumudu changamoto mnazozikabili.
Naomba nichukue fursa hii kuwaasa taasisi za kifedha hapa
nchini kuongeza juhudi za kutoa mikopo kwa wanawake wajasiriamali, na pia
kuhakikisha kuwa riba zinazotolewa zinaruhusu wajasiriamali hawa kukua
kibiashara na si kuwakandamiza.
Ni
muhimu pia kwa wanawake wajasiriamali kuchangamkia fursa zinazotolewa na
taasisi za kifedha, nawaomba mikopo mnayopata muitumie kwa umahiri ili kuweza kufikia
malengo yenu katika ukuaji wa biashara.
Usawa wa kijinsia katika elimu na fursa za kiuchumi
imeendelea kuwa changamoto kubwa, ambayo wanawake duniani kote wamekuwa
wakipambana nayo. Hatua kubwa mpaka sasa
imefikiwa katika kuwakomboa wanawake kutoka kwenye umasikini.
Hata hivyo, bado wanawake wengi zaidi
wanakabiliwa na ukosefu wa fursa za elimu na umasikini wa kipato. Hivyo, juhudi kubwa zinahitajika kwa kila
mmoja wetu kufanikisha majukumu yetu katika fursa tulizonazo.
Tunatambua kabisa kwamba wanawake
wanaposhiriki kikamilifu katika shughuli za jamii, uchumi wa nchi hukua
zaidi. Siku ya leo ni nyenzo muhimu sana
katika kuwawezesha wanawake kujifunza kutoka kwa wengine walivyofanikiwa,
kubadilishana uzoefu na kuelimishana.
Napenda kuwakumbusha juu ya nguvu kubwa ya wanawake katika
kulisaidia Taifa letu kuimarika kiuchumi na kujitegemea. Ushiriki wenu katika mapinduzi ya kiuchumi,
uwe ni kipaumbele katika mipango yenu ya kila mwaka. Bidhaa na huduma mnazotoa muongezee uthamani
wake ili tuweze kumudu changamoto za ushindani katika soko la ndani na
dunia.
Tujitahidi biashara zetu
tuziendeshe kwa kutumia teknolojia bora, na kufuata ushauri wa wataalamu wa
ujasiriamali. Tutumie vyuo vya mafunzo
vilivyopo hapa nchini kujiendeleza, vyuo ambavyo tayari vinatoa ujuzi
mbalimbali kwenye ujasiriamali. Pia tuwe makini katika kutunza mitaji yetu na
kutumia huduma za kifedha vyema ili kuimarisha biashara zetu.
Vile vile napenda kutumia fursa hii kuwaasa
akinamama kwa ujumla, kutokatishwa tamaa na vikwazo mnavyokumbana navyo katika
maisha. Ni muhimu tuwe na mipango mizuri
ya maendeleo, na kutumia muda wetu vyema ili kujiletea mabadiliko katika kila nyanja,
tusibweteke na kupoteza wakati.
Baada ya kusema haya napenda kutoa pongezi zangu za dhati kwa
kamati ya maandalizi, uongozi na wafanyakazi wa Maznat Bridal Care, kwa sherehe
nzuri iliyofana sana. Aidha, nawapongeza
wanawake mliofika hapa leo kwa usikivu na uchangamfu wenu, pamoja na watoa
huduma na burudani mbalimbali. Nawaomba
tuendelee kudumisha ushirikiano wetu katika kukuza uchumi wa taifa letu. Natangaza sasa sherehe za miaka kumi ya
Maznat zimefunguliwa rasmi.
Ahsanteni sana kwa kunisikiliza.




















No comments:
Post a Comment