Mbuzi wakichuana ili kumpata mshindi katika mwashindano ya mbio za mbuzi za hisani za mwaka jana. (Picha ya Maktaba)
*****************************************************
‘Mbuzi Mmoja tu,
Anaweza Kuleta Mabadiliko’
Waandaji
wa mbio hizo maarufu nchini wamesema jijini hapa leo kuwa kwa sasa mbuzi
watakaoshiriki mbio hizo wako kwenye kambi za mazoezi huku zawadi kemkem za
kuvutia zikiwa zimeandaliwa kwa mwaka huu.
“Tunachokihitaji
kwa sasa ni uwepo wa mashabiki watakaohudhuria tukio hilo la kufurahisha na
hivyo kutusaidia kufikia lengo tulilojiwekea la kusanya shilingi bilioni moja kwa
ajili ya taasisi mbalimbali za kujitolea nchini,” Mwenyekiti wa Kamati ya
Maandalizi, Mama Karen Stanley alisema.
“Siku
hiyo tumeandaa sehemu mahsusi kwa ajili ya aina mbalimbali ya vyakula vya
kuvutia kutoka sehemu maarufu zinazohusika na mapishi jijini Dar kama Rose
Garden, Arca di Noe, Black Tomato na Q Bar.
“Pia tutakuwa na eneo lililokarabatiwa kwa ajili ya michezo ya watoto
litakalowafanya watoto watakaofika kufurahi na kuikumbuka siku hiyo. Lipo eneo
jingine jipya kwa watoto wadogo zaidi huku eneo jingine lililotayarishwa na Neverland Playgroup
and entertainment kwa ajili ya watoto wakubwa zaidi litakalokuwa na michezo
kama sarakasi, ngoma, kucheza muziki na wachekeshaji kutoka asasi ya Kigamboni Community Centre.”
Tukio
hilo ka kifamilia la kila mwaka litafanyika Juni Mosi mwaka huu kwenye eneo la Green,
mtaa wa Kenyatta kuanzia saa sita mchana hadi saa 11.30
jioni. Gharama za tiketi ni Sh 5,000 kwa watu wote na zitauzwa getini.
Mbio
hizo za mbuzi za hisani zinafanyika kwa mara ya 13 mwaka huu. Tangu
yalipoanzishwa mwaka 2001, tayari zaidi ya shilingi milioni 660 zimekwisha
kusanywa kwa ajili ya mashirika na taasisi mbalimbali za kujitolea nchini.
Mwaka
jana tukio hilo liliweka rekodi kwa kukusanya shilingi milioni 115 kwa kwa
ajili ya mashirika 15, huku wahudhuriaji wakifika 4,200 na kulipa kiingilio
getini.
Mama
Stanley alisema: “Mwaka huu tunatarajia kufanya makubwa zaidi. Tunafuraha ya
kuwa na wadhamini wengi muhimu sana, ambao ndio uti wa mgongo wa tukio lenyewe.
Bila wao hakika tusingekuwa hapa. Kwa namna ya pekee yunatoa shukrani kwa
wadhamini wa mbio hizo Southern Sun, Coca-Cola, Tanzanian Breweries Limited,
Mantra Tanzania, Erolink, FNB na Symbion.
“Lakini
ukweli ni kwamba bila ujio wa watu wa kawaida, mashabiki kutoka sehemu mbalimbali
za Dar, wenyeji na wageni, kushuhudia mbio hizo za aina yake kusingekuwa na
maana yoyote. Kwa hiyo karibuni nyote, msiisahau siku hiyo ya ajabu kabisa!”
Miongoni
mwa zawadi kubwa kwa mwaka huu ni tiketi ya kwenda Ulaya na kurudi
itakayotolewa na SWISS, safari ya kwenda kwenye mbuga ya wanyama ya Selous na
kifurushi cha kupata mtandao wa Intaneti kwa mwaka mzima kutoka UhuruOne kikiambatana
na vifaa na uunganishaji.
Dhana
ya mwaka huu, ‘Viumbe wa Baharini na Mabaharia’,
inaweza kuvutia wengi wanaopenda kuingia kwenye mashindano ya mavazi ya kuvutia
huku kukiwa na zawadi nono kwa kundi litakalovaa vyema. Kutakuwa pia na
shindano la mavazi maalumu kwa watoto na zawadi kwao.
Mama
Stanley alisema: “Ukija umevaa kwa mtindo wa nguva au baharia, au hata ukiwa
kawaida tu utafurahia mambo tuliyokuandalia mwaka huu.”
Kwa habari zaidi tembelea tofutti yetu; www.goatraces.com
Kwa
waandishi wa habari wasiliana na Peter Mgongo kwa simu namba 0784 765454 au mgongo@gmail.com
Kwa
maelezo yote kuhusu masuala ya habari wasiliana na Emma Pearson (Mjumbe wa
Kamati anayeshughulikia masuala ya Habari na Mahusiano) simu 0768 912933 au ekpea@yahoo.co.uk
Maelezo kwa Wahariri:
- Mwenyekiti wa Kamati ya ‘Goat Races’, Karen Stanley anapatikana kwa mahojiano ikiwa atahitajika.
- Picha pia zinapatikana kwa maombi rasmi.
- Jinsi mbio hizo zinavyofanyika:
Kuna aina saba za mashindano. Kila moja
hudhaminiwa na wamiliki wa mbio hizo ambao kwa mwaka huu ni:
The
Marvelous Mantra Mile
The
Southern Sun Fillies Frolic
The
Symbion Sweepstakes
The
Kilitime Stakes
The
Erolink Racy Recruits
The FNB
Champions Cup
The
Coca-Cola Open Happiness Sweepstakes
Hawa humlipia mbuzi mmoja katika shindano
moja. Mbuzi wao akishinda, wanakuwa na nafasi ya kupata zawadi kubwa. Wengi
huungana na rafiki au jamaa zao na kuwa wamiliki wa pamoja wa mbuzi.
Wote hupata nafasi ya kuingia kwenye eneo
maalumu na kupata nafasi nzuri ya kumshangilia mbuzi wao, na kupata vinywaji na
chakula bure kwa hisani ya Southern Sun Hotel, Tanzania Breweries Ltd, Tanzania
Distilleries Ltd, na Coca-cola.
4
Mbio
hizi zilianza jijini Dar es Salaam mwaka 2001 shukrani kwa muasisi Paul
Joynson-Hicks. Alipata wazo hilo kutoka Uganda ambako wafanyabiashara walibuni
wazo hili ili kukusanya fedha za hisani.
Zawadi
maalumu kwa mwaka huu za bahati nasibu:
- The Raffle Prizes 2013 – tiketi ni Sh 2,500 na zitauzwa siku hiyo.
·
SWISS – tiketi
moja ya kwenda na kurudi Ulaya
·
Selous
Great Water Lodge – safari ya Selous
·
UhuruOne – kuunganishwa
na internet ya bure kwa mwaka mzima
·
Sea Cliff
Resort and Spa, Zanzibar – malazi hoptelini hapo kwa watu wawili na
tiketi mbili za kwenda na kurudi Zanzibar kutoka Coastal Airlines
·
Benetton
Gems – heleni za Tanzanite zenye thamani ya dola 1,000
·
Ras
Kutani – malazi ya siku mbili
·
Arena Gym
(zawadi mbili) – uanachama
wa gym kwa mwezi mmoja, massage ya saa moja pale Arena Spa na huduma za Saluni.
·
Anantara
Spa – massage kwa mtu na mwenza wake
·
Toyota
Tanzania – goodie bag
·
The
Fitness Centre – uanachama wa gym kwa miezi mitatu
·
Akemi
Revolving Restaurant – vocha ya chakula cha jioni ya thamani ya sh 250,000
·
Shrijees
Supermarket – zawadi mbalimbali
·
TDL – zawadi
mbalimbali
1.
Vituo vitakavyofaidika
na mbio za mwaka huu ni:
- Matumaini
Day Care Center for Disabled Children - http://www.holyuniontanzania.co.ok/
- Zanzibar
Outreach Program (ZOP) –
- Bibi
Jann's Centre
–
- Fahari
Zanzibar
–
- CCBRT
(Comprehensive Community Based Rehabilitation in Tanzania) - http://www.ccbrt.org.tz/
- Malaika
Kids
–
- AC-AF –
- Foxes' Community and
Wildlife Conservation Trust –
- The
Daughters of Mary Immaculate and Collaborators (DMI)
No comments:
Post a Comment