Habari za Punde

*RED COAST, KARIAKOO, SAIGONI KUANZIA NYUMBANI RCL


Upangaji ratiba (draw) ya Ligi ya Mabingwa wa Mikoa (RCL) umefanyika leo (Mei 7 mwaka huu) huku mabingwa wa mikoa ya Dar es Salaam (Red Coast), Lindi (Kariakoo) na Kigoma (Saigoni) wakianzia nyumbani katika ligi hiyo itakayoanza Mei 11 au 12 mwaka huu.

Ligi hiyo itachezwa kwa mtoano kwa mtindo wa nyumbani na ugenini ambapo mwenyeji atapanga tarehe ya mechi ambazo zinatakiwa kuchezwa kati ya Jumamosi au Jumapili. Mechi za marudiano katika raundi hiyo ya kwanza zitachezwa kati ya Mei 18 na 19 mwaka huu.

Katika upangaji huo ulioshuhudiwa na waandishi wa habari kwa niaba ya klabu husika, mabingwa wa Mkoa wa Shinyanga (Stand Ngaya FC) wamepita moja kwa moja hadi raundi ya pili itakayochezwa kati ya Mei 25 na 25 mwaka huu wakati mechi za marudiano ni kati ya Juni 1 na 2 mwaka huu.

Raundi ya tatu itachezwa kati ya Juni 8 na 9 mwaka huu wakati marudiano ni Juni 15 au 16 mwaka huu. Raundi ya nne itachezwa kati ya Juni 22 au 23 mwaka huu wakati marudiano ni Juni 29 au 30 mwaka huu. Raundi ya tano ni kati ya Julai 6 na 7 mwaka huu na marudiano ni Julai 13 au 14 mwaka huu.

Timu tatu ndizo zitakazopanda kucheza Ligi Daraja la Kwanza (FDL) msimu ujao, ambazo ni ya kwanza nay a pili wakati timu ya tatu itapatikana kwa timu zilizoshindwa hatua ya nusu fainali kucheza zenyewe kwa zenyewe. Washindi wa nusu fainali nao watacheza wenyewe kwa wenyewe ili kupata bingwa wa RCL ambaye atakabidhiwa kombe la ubingwa.

Ligi hiyo inashirikisha mabingwa kutoka mikoa 27 ya kimpira ambapo katika raundi ya kwanza wanaanza mabingwa 26, raundi ya pili ni mabingwa 14 wakijumuisha na bingwa wa Shinyanga ambaye katika draw ameingia moja kwa moja katika hatua hiyo.

Raundi ya tatu itashirikisha timu saba zilizosonga mbele pamoja na moja yenye uwiano mzuri wa matokeo ili kufanya jumla ya timu nane. Raundi ya nne itakuwa na timu nne. Wakati raundi ya tano itakuwa ni kumpata bingwa na mshindi wa tatu.

Katika upangaji huo wa ratiba mechi za raundi ya kwanza (timu ya kwanza ikianzia nyumbani) itakuwa kama ifuatavyo; Red Coast vs Abajalo, Kariakoo vs Mtwara, Friends Rangers vs Kiluvya United,  TECKFOLT FC vs African Sports, Machava FC vs Flamingo SC, Gunners United vs Manyara na Simiyu vs Magic Pressure FC.

Nyingine ni Polisi Jamii Bunda FC vs UDC FC, Geita vs Biharamulo SC, Saigoni SC vs Tabora, Katavi Warriors vs Rukwa United, Mji Njombe vs Mbinga United na Kimondo FC vs Iringa.

Mechi zitachezwa katika viwanja vya makao makuu ya mikoa, vinginevyo kuwepo na maombi rasmi ambayo yatakubaliwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).

      TANZANIA FOOTBALL FEDERATION    
          Affiliated to FIFA, CAF and CECAFA    
          Karume Memorial Stadium, Uhuru/Shaurimoyo Rd – Ilala    
          P.O. Box 1574, Dar Es Salaam, Tanzania    

        Telefax: +255 22 2861815, Email:tfftz@yahoo.com, Website: www.tfftanzania.com

 
 

MUUNDO WA LIGI YA MABINGWA WA MKOA - 2013
   
     
  HATUA YA I     HATUA YA II
No. TEAMS   No. TEAMS
1 TEMEKE  Vs  ILALA   27 WIN 12  Vs  WIN  3 4
2 ILALA  Vs  TEMEKE      
3 LINDI   Vs  MTWARA   28 WIN  &   4   Vs  WIN  &  2
4 MTWARA  Vs  LINDI      
5 KINONDONI   Vs  PWANI   29 WIN  6  Vs  WIN  7 & 8
6 PWANI    Vs    KINONDONI      
7 MOROGORO     Vs     TANGA   30 WIN  7   &  8  Vs  5 &  6
8 TANGA     Vs     MOROGORO      
9 KILIMANJARO    Vs   ARUSHA   31 WIN 9  & 10  Vs  WIN  11 & 12
10 ARUSHA   Vs   KILIMANJARO      
11 DODOMA    Vs     MANYARA   32 WIN  11 & 12  Vs  WIN  9 & 10
12 MANYARA    Vs     DODOMA      
13 SIMIU VS SINGIDA   33 WIN  13  &  14   Vs  SIMIYU
14 SINGIDA VS SIMIU      
  BY - SHINYANGA   34  SIMIYU  Vs  WIN 13 & 14
15 MARA VS MWANZA   35 WIN  15 & 16  Vs  WIN  17 & 18
16 MWANZA VS MARAS      
17 GEITA VS KAGERA   36 WIN 17 & 18  Vs  WIN  15 & 16
18 KAGERA VS GEITA      
19 KIGOMA VS TABORA   37 WIN  19 & 20  Vs  WIN 21 & 22
20 TABORA VS KIGOMA  
 
 
     
21 KATAVI VS RUKWA   38 WIN  2122  Vs  WIN 19 & 20
22 RUKWA VS KATAVI      
23 NJOMBE  Vs  RUVUMA   39 WIN  23 & 24  Vs  WIN  25 & 26
24 RUVUMA   Vs  NJOMBE      
25 MBEYA VS IRINGA   40 WIN 25 & 26  Vs  WIN  23 & 24
26 IRINGA VS MBEYA      
  HATUA YA III     HATUA YA IV    
41 WIN 2728  Vs  WIN  29 30   49 WIN  41 & 42   Vs  WIN  43 & 44
         
         
42 WIN  29 & 30   Vs  WIN 27  &  28   50 WIN  43  44  Vs  WIN 41 & 42  
          WINNER 49 & 50 (1ST)
43 WIN  31  & 32  Vs  WIN  33 & 34   51 WIN  45 & 46   Vs  47 &  48
         
44 WIN  33   & 3 4  Vs  31 &  32   52 WIN 47  & 48  Vs  WIN  45 & 46  
          WINNER 51 & 52 (2ND)
45 WIN 35  & 36  Vs  WIN  37 & 38   53 LOOSER   49   &   50  
         
46 WIN  37  &   38   Vs  WIN  35  &  36   54 LOOSER  51  52   
          WINNER 53 & 54 (3RD)
47 WIN  39  40  Vs  BEST LOOSER   55 WINNER  51   &  52 
         
48 BEST LOOSER  Vs  39 &  40
   
         
         

No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.