Habari za Punde

*SH. BILIONI 876.3 KUTATUA MSONGAMANO WA MAGARI JIJINI DAR

Magari yakiwa katika foleni eneo la Kijitonyama mbele ya Millenium Tower, kutokana na eneo hilo kujaa maji ya mvua kubwa zilizonyesha jijini Dar es Salaam, juzi.
**************************************
Na Immaculate Makilika- Maelezo

SERIKALI imesema   inatekeleza miradi ya kupunguza msongamano wa magari katika jiji la Dar es Salaam yenye thamani ya sh. bilioni 876.336   katika barabara ya Al Hassan Mwinyi ambapo watumiaji wa barabara hiyo hutumia takribani saa moja na nusu kufika Osterbay polisi hadi daraja la Salender hususani mida ya asubuhi saa moja hadi saa tatu.

Hayo  yalisemwa jana Bungeni na  Naibu Waziri wa Ujenzi   Gerson  Lwenge Naibu  wakati    akijibu swali  Mbunge  wa Jimbo la  Temeke  Abasi Zuberi Mtemvu  lililouliza kuwa  Je,Serikali inaweza kutoa ufafanuzi juu ya ufumbuzi wa tatizo la msongamano huo?

Alisema   kuwa  inayolenga kutatua tatizo hilo ,ikiwemo miradi ya kupunguza msongamano wa magari katika jiji hilo ambayo ni  kama ifuatavyo;.Barabara ya Kimara –Kivukoni (fire),Fire-Kariakoo na Magomeni –Morocco (Sh.  bilioni 240),Karakana na vituo vya mabasi yaendayo kwa haraka (BRT) pamoja na kuhamisha nguzo za umeme(sh. bilioni 47.90).

Nyingine ni  Barabara ya Mwenge – Tegeta(sh.  bilioni 88.00),Barabara ya Kilwa (Kilwa Road) Bendera Tatu-Mbagala Rangi Tatu ,(sh.  bilioni 35.16),Daraja la Kigamboni (sh. 214.64).Flyover ya TAZARA,Serikali ya Japani imetoa msaada wa fedha kwa ajili ya usanifu,.Barabara ya Gerezani (Bendera –Tatu-KAMATA),Serikali ya Japani imetoa  msaada wa fedha kwa  ajili ya ujenzi.

Barabara ya Mandela (sh. bilioni 61.25) na.Barabara ya  Wazo Hill –Bagamoyo-Msata (sh. bilioni 89.61).

Waziri  huyo  alisema  ujenzi wa mabasi yaendayo haraka(BRT) kutoka Morocco kwenda Magomeni hadi Kivukoni na Kimara yatapunguza msongamano wa magari kati ya Osterbay Polisi na Daraja la Salender.

 Aliongeza kuwa katika mipango ya baadae ,Serikali itaangalia uwezekano na kujenga barabara ya juu  (viaduct) pande zote za daraja ,kujenga daraja lingine pembeni mwa daraja la Salender au kujenga njia mbadala (salender bridge Bypass) kutokea Kenyata Drive  kuunganisha na Ocean Road.

* SERIKALI KUFUFUA KILIMO CHA KAHAWA KILIMANJARO

 SERIKALI imesema  kuwa imeandaa mkakati wa kuendeleza  tasnia ya kahawa ( Tanzania Coffee Industry Development  Strategy,2012-2022) kwa lengo la kuendeleza kilimo cha  zao  hilo  nchini kupitia Bodi ya kahawa  nchini  na kwa kushirikiana na wadau wa sekta ya hiyo.

Aidha  Serikali imefafanua  kuwa hatua hiyo ni  kuongeza uzalishaji ,tija na ubora wa kahawa Kitaifa ili kuboresha mapato ya wakulima wa zao hilo  katika mikoa mbalimbali inayolilima  ikiwemo mkoa wa Kilimanjaro .

Kauli hiyo ilitolewa leo Bungeni na Waziri wa  Nchi Ofisi ya Mahusiano  na  Uratibu  Steven Wassira kwa niaba  Waziri wa Kilimo ,Chakula na Ushirika , Chrisopher Chiza , wakati akijibu swali la  Grace   Kiwelu(Mbunge Viti Maalum-CHADEMA) aliyeuliza  Je,Serikali ina mpango gani  madhubuti na mahsusi wa kufufua kilimo cha Kahawa mkoani Kilimanjaro  ambacho  kwa miaka mingi kimekua tegemeo kwa wananchi  wa Kilimanjaro na mhimili mkubwa kwa uchumi wetu wa Taifa letu.

 Alisema malengo mahsusi ya mkakati huo ni pamoj ana kuongeza na uzalishaji  wa kahawa safi kutoka wastani wa sasa wa tani 50,000 kwa  mwaka hadi kufikia tani  100,000 ifikapo mwaka 2022 na kuongeza ubora  wake  ili kupata bei ya ziada katika masoko ya nje kutoka wastani wa asilimia  35 hadi kufikia wastani wa asilimia 70 ifikapo  mwaka 2022.

Aidha Wassira alisema maeneo muhimu katika mkakati huo ni pamoja na kuimarisha huduma za ugavi  ili wakulima wazingatie kanuni bora za kilimo,kushirikiana na Taasisi ya Utafiti wa Kahawa (TaCRI) ili kuhakikisha  upatikanaji wa miche bora ya kahawa ,pamoja  na kuongeza matumizi ya viwanda vya kati vya kuitayarisha  ili kuongeza ubora wa zao hilo na hivyo wakulima kunufaika na bei nzuri.

No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.