Habari za Punde

*RAIA WAWILI WA SENEGAL WAUAWA ITALIA

Mwanamume mmoja raia wa Italia alifyatua risasi katika maeneo mawili ya soko na katikati mwa mji wa Florence,na kuwaua wafanyabiashara wawili raia wa Senegal pamoja na kuwajeruhi watu wengine watatu. 

Mshambuliaji huyo, Gianluca Casseri mwenye umri wa miaka 50, ni mfuasi wa kundi moja lenye kufuata siasa za mrengo wa kulia, vyombo vya habari vya nchini Italia vimeripo.

Muuaji huyo aliwaua wanaume wawili na kumjeruhi mwingine katika medani ya Dalmazia kabla ya kufyatua risasi katika medani ya San Lorenzo, na uwajeruhi wengine wawili.

Ripozti zinasema kuwa muuaji huyo,Casseri, baadaye  alipatikana akiwa tayari amejiua baada ya kujipiga risasi mwenyewe, polisi wanasema.

Rais wa Italia, Giorgio Napolitano, amelaani vikali chuki hizo zinazoendelea kujitokeza na ambazo hazina msingi na amewataka maofisa wa Italia pamoja na jamii kwa jumla kukabiliana na watu wasioweza kuwastahimili wenzao na kuhakikisha kuwa kuna uwazi na mshikamano katika nchi hiyo.

Meya wa mji wa Florence alielezea shambulio hilo kuwa ni kama la mtu aliyekosa muelekeo.

"haya ni matendo ya muuaji mmoja - mwendawazimu na muuaji mwenye ubaguzi wa rangi," Matteo Renzi alisema, akiongeza kuwa kitendo kama hiki si sifa nzuri kwa mji huo na kimewastusha watu wengi.

No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.