• Serikali yasita nini kuweka wazi ugonjwa wa Mwakyembe?
Na Mwandishi wetu
Naibu Waziri wa Ujenzi, Dk. Harrison Mwakyembe
Naibu Waziri wa Ujenzi, Dk. Harrison Mwakyembe
Naibu Waziri wa Ujenzi, Dk. Harrison Mwakyembe
NAANDIKA makala hii kwa uangalifu mkubwa nikitambua kwamba ni mfano wa makala ambazo ukishaandika na kuchapishwa gazetini, kesho yake unaweza kufuatwa nyumbani na maofisa wa polisi au wa Usalama wa Taifa na kutakiwa utoe ushahidi wa uliyoyaandika.
Najihami mapema kwao kwamba hakuna jambo lolote jipya katika makala hii linaloweza kuwachochea kunifuata; maana yote yalishawekwa wazi kwenye vyombo vingi vya habari, na wala hayakupatwa kukanushwa.
Kwa hiyo, hakuna jipya hapa mbali ya hoja zangu ambazo naamini zinafikirisha. Kama bado watanifuata, basi, lengo lao litakuwa ni kunitisha (mimi na wengine) ili nisiandike tena kuhusu suala hili.
Ndugu zangu, suala ninalojaribu kuliandika kwa tahadhari kubwa hapa ni la masahibu yaliyomkuta Naibu Waziri wa Ujenzi, Mbunge wa Kyela na mmoja wa makamanda wa vita dhidi ya ufisadi nchini, Dk. Harrison Mwakyembe.
Ni karibu miezi miwili sasa tangu Dk. Mwakyembe arejee kutoka India alikopelekwa kwa matibabu ya ugonjwa ambao mpaka sasa umma haujaelezwa rasmi jina lake.
Nimekuwa nikisita kwenda nyumbani kwake kumpa pole, kwa sababu mwenzetu wa Raia Mwema tuliyemtuma kwenda kumuona mara aliporejea kutoka India, alitupa simulizi ya kusikitisha juu ya hali yake. Na mimi kwa udhaifu wa moyo wangu, nahofia ‘presha’ inaweza kunipanda nikimuona, na pengine kuanguka hapo hapo nyumbani kwake.
Kusita kwangu kwenda kumuona na kumpa pole kuliimarishwa zaidi na habari niliyoisoma kwenye gazeti la Tanzania Daima, toleo la Januari 4, 2012, ukurasa wa kwanza, iliyobeba kichwa kinachosomeka “Dk. Mwakyembe ana siri nzito”.
Kwenye habari hiyo ilielezwa kwamba afya ya Mwakyembe inasikitisha; kwani licha ya kupata matibabu nchini India na kuendelea na tiba hiyo hapa nchini, hali yake si ya kuridhisha.
Kwa mujibu wa habari hizo, kucha za vidoleni na miguuni zimeoza na zina rangi nyeusi, miguu na mikono yake imepasuka mithili ya mtu mwenye magamba ambayo wakati mwingine hutoa damu.
Si hivyo tu. Tumeelezwa pia kwamba kichwani hana nywele; kwani zimepukutika zote ikiwa ni pamoja na nyusi za kope. Hali hii humfanya muda wote avae kofia kichwani na glovu mikononi na hata miguuni kuhifadhi viungo vyake hivyo.
Maelezo hayo ya hali ya Dk. Mwakyembe hayanipi mimi, mwenye moyo dhaifu, ujasiri wa kwenda kumuona, na naishia tu kumwombea kwa Mwenyenzi Mungu kwenye sala zangu. Niseme tu kwa Dk. Mwakyembe kupitia makala hii: Hang in there brother, pambana kuokoa maisha yako. Mungu atakusaidia.
Ukweli ni kwamba, kwa yaliyomsibu Dk. Mwakyembe; hata kama atapona kabisa, hawezi kuwa Mwakyembe yule yule tuliyemzoea.
Kwa hakika, atahitaji miaka mingi ya tiba ya kiroho (spiritual healing) na ushauri nasaha kutoka kwa mabingwa wa dunia wa fani hiyo kuweza kusahau yote yaliyomsibu na kuendelea na maisha yake kama kawaida. Huo ndio ukweli wa kipimo cha masahibu yaliyomkuta.
Nikitafakari masahibu hayo yaliyomkuta kamanda huyu wa vita dhidi ya ufisadi, nahisi kuna kitu hakiko sawa katika namna Serikali ya Rais Jakaya Kikwete inavyolishughulikia suala la kiongozi huyo wa Serikali.
Hata hivyo, kabla sijakizungumzia kitu hicho, nianze kwa kumshukuru na kumpongeza Rais Kikwete kwa hatua aliyoichukua ya haraka ya kumpeleka India Dk. Mwakyembe siku alipomtembelea nyumbani kwake na kusononeshwa na hali aliyomkutanayo.
Habari za uhakika nilizonazo ni kwamba Rais Kikwete alihuzunishwa mno na hali ya Dk. Mwakyembe kiasi kwamba alianza hapo hapo sebuleni kwa Mwakyembe kumpigia simu Waziri Magufuli na Waziri wa Afya na kuwapa maelekezo kwamba anataka kuona Dk. Mwakyembe anapelekwa India kwa matibabu ndani ya kipindi cha saa 24! Na ndivyo ilivyokuwa.
Kwa mtazamo wangu; namna Kikwete alivyoishughulikia kwa haraka safari hiyo ya India ya Mwakyembe, ni uthibitisho wa kutosha kwamba Rais wetu ni mwenye huruma na upendo.
Kikwete anaweza akawa na udhaifu wake kiuongozi; lakini ukweli unabaki pale pale kwamba yu mwenye huruma na mpole, na hizo ni sifa zinazotunisha thawabu zake kwa Mungu!
Kuhusu suala la mushkeli ninaouona katika namna ambavyo Serikali yake inavyolishughulikia suala la Mwakyembe, napenda nikite kwenye huu ububu wa Serikali katika kuueleza umma nini hasa kilimsibu jemadari huyo wa vita dhidi ya ufisadi.
Kwa jinsi ninavyofahamu, Dk. Mwakyembe amerejea nchini na ripoti ndefu ya madaktari wa India waliomtibu ambayo inaeleza nini hasa chanzo cha kuzorota kwa hali yake ya afya, na ripoti hiyo ameiwasilisha serikalini; kwani ni Serikali ndiyo iliyompeleka India kwa matibabu. Hili halina ubishi.
Linaloweza kuwa na ubishi lakini unaojadilika, ni hili ambalo nimelijenga katika hisia. Hisia zangu ni kwamba Dk. Mwakyembe mwenyewe anapenda Serikali iweke hadharani ripoti hiyo ya madaktari wake aliyorejeanayo kutoka India. Kwa maneno mengine; Dk. Mwakyembe anataka umma uelezwe nini kilichomsibu.
Baadhi ya watu anaowaamini waliopata kumtembelea nyumbani kwake, si tu amewadokezea kilichomo kwenye ripoti hiyo, lakini pia amesema kwamba kama Serikali itaendelea na ububu wa kutoitoa hadharani, basi, yeye ataeleza umma siri iliyomo kwenye ripoti hiyo ya madaktari wa India.
Sasa kama nipo sahihi kwamba Dk. Mwakyembe mwenyewe anataka umma uelezwe kilichomo kwenye ripoti ya madaktari hao wa India, sielewi ni kwa nini Serikali inasita kufanya hivyo.
Majibu ambayo Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Blandina Nyoni, alilipa gazeti la Majira (toleo hilo la Januari 4); kwamba eti suala la ugonjwa wa Mwakyembe aulizwe mwenyewe Mwakyembe, hayaridhishi na hayana busara ndani yake.
Ni kweli kwamba ugonjwa wa mtu ni siri ya mgonjwa mwenyewe; lakini vipi kama mgonjwa mwenyewe anataka siri ya ugonjwa wake iwekwe hadharani? Na tunao mfano wa ridhaa ya Rais Kikwete kwa daktari wake kuelezea hali ya afya yake (ugonjwa) mbele ya waandishi wa habari. Uamuzi uliofuatia na tukio la yeye (Kikwete) kuanguka jukwaani, mkoani Mwanza.
Isitoshe; hapa hatuzungumzii mgonjwa wa kawaida. Hapa tunazungumzia mgonjwa ambaye ni Naibu Waziri, Mbunge, mwanaharakati wa haki za binadamu na mmoja wa makamanda wa vita dhidi ya ufisadi.
Isitoshe; hapa vilevile tunamzungumzia kiongozi wa ngazi ya waziri ambaye waziri mwingine mwandamizi serikalini, na ambaye ni mpambanaji mwenzake katika vita dhidi ya ufisadi (Samuel Sitta) tayari alishautangazia umma kwamba kinachomsibu Dk. Mwakyembe ni sumu.
Na Samuel Sitta si pekee kuutangazia umma hivyo kwenye kipindi cha Dakika 45 cha ITV; kwani Mwenyekiti wa Halmshauri ya Kyela naye alisema hivyo hivyo na kunukuliwa na magazeti siku alipomtembelea Mwakyembe nyumbani kwake aliporejea kutoka India.
Watu hawa wawili – Sitta na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kyela, ni watu walio karibu sana na Dk. Mwakyembe, na hivyo yawezekana kabisa dhana hiyo ya kupewa “sumu” imetoka kwa Mwakyembe mwenyewe (from the horse’s mouth).
Sasa, kama mazingira ni haya, kwa nini Serikali haioni umuhimu wa kuiweka hadharani ripoti hiyo ya madaktari wa India ili ukweli rasmi ufahamike? Inaona ugumu gani kufanya hivyo?
Kama, kwa mfano, (narudia maneno ‘kwa mfano’ ) kilichomsibu ni kuwekewa sumu ya polonium 210 kama ile iliyotumika kumuua kachero wa Urusi, mjini London, Alexander Litvinenko, basi umma uambiwe; maana katika u-Mafia ambao tumeufikia hivi sasa hapa nchini kwetu, hilo nalo halitatushangaza sana.
Lakini kama pia kilichomsibu si sumu, ni logic (mantiki) umma ukatangaziwa ili fikra hizo kwamba Dk. Mwakyembe aliwekewa sumu ziondoke vichwani mwa Watanzania.
Hivi kuna tatizo gani Waziri wa Afya akaitisha mkutano na waandishi wa habari na akawaeleza, japo kwa ufupi, kilichomo kwenye ripoti hiyo ya madaktari wa India?
Hata kama ripoti inasema kuwa tatizo ni sumu aliyopewa, kuna hatari gani watu kufahamishwa hivyo; hasa kama jeshi la polisi nalo litasema kwamba linaanzisha uchunguzi kujua namna sumu hiyo ilivyompata Mwakyembe?
Nauliza maswali haya yote kwa sababu suala la Mwakyembe si la kawaida, na linaweza kuwa ni tukio la aina yake katika historia ya miaka 50 ya uhuru wetu.
Nasema hivyo kwa sababu, hata kabla hajakumbwa na masahibu haya ya sasa ya mwili kubabuka na kuota magamba; huku nywele na kope zikipukutika, Dk. Mwakyembe alishautangazia umma kwamba maisha yake yamo hatarini.
Huyu ni mbunge na naibu waziri ambaye ataingia katika vitabu vya kumbukumbu kwamba ni mbunge wa kwanza nchini kuandika rasmi barua kwa Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) akilalamika kwamba kuna wauaji wa nje wamekodishwa kuja kumuua, na kisha akatoa maelezo zaidi jinsi walivyomfuatilia kwa gari alipokuwa safarini.
Sikumbuki kama katika historia ya Tanzania ya miaka 50 iliyopita kuna mbunge au waziri aliyemwandikia barua rasmi IGP akimtaarifu kuwa kuna wauaji wa kigeni wanamfuatilia kwa lengo la kumuua. Kama yupo, nikumbusheni.
Lakini japo IGP wetu alikiri kuipokea barua hiyo ya Mwakyembe, hakuna maelezo yaliyotolewa mpaka sasa kama kuna mtu yeyote aliyekamatwa kuhusiana na madai hayo ya Mwakyembe au hata kuuelezea tu umma upelelezi wa suala hilo ulipofikia.
Sasa wakati umma ukisubiri kuelezwa na IGP maendeleo ya uchunguzi wa malalamiko hayo yaliyowasilishwa na Mwakyembe juu ya watu wanaotaka kumuua, ghafla anakumbwa na ugonjwa huo wa ajabu na kukimbizwa India – ugonjwa ambao yeye mwenyewe anaamini chanzo chake ni sumu!
Sasa, katika hali hii, na katika mazingira haya ambapo bado hali ya afya ya Naibu Waziri huyo haijatengemaa; licha ya kupelekwa India kwa matibabu, Serikali haioni lojiki kuiweka sasa hadharani ripoti hiyo ya madaktari wa India waliomtibu ili ukweli ufahamike?
Nionavyo mimi, ni busara Serikali ikatoa tamko sasa kuhusu kilichomsibu Mwakyembe na kuweka hadharani chanzo cha ugonjwa unaomsumbua wakati Mwakyembe mwenyewe angali hai ili awe na fursa ya kukubaliana na hicho kitakachoelezwa na Serikali au kukikataa.
Mungu aepushie mbali, lakini kama Mwakyembe atafariki na kutangulia mbele ya haki, chochote ambacho Serikali itakitamka baada ya yeye kufa kuhusu kilichomuua, hakitaaminika kwa jamii.
Kwa maneno mengine; ni vyema Serikali itamke sasa kuhusu chanzo cha ugonjwa wa Mwakyembe; vinginevyo akifariki, itabidi ifunge mdomo milele!
Nimalizie makala yangu kwa kumwambia tena Dk. Mwakyembe: Hang in there brother, pambana kuokoa maisha yako. Mungu atakusaidia utapona. Watanzania wanakupenda kwa jinsi ulivyojitolea mhanga kuwatetea kwa kupambana na ufisadi.
Kwa upande wa Serikali yetu, nisisitize tena kwamba ina wajibu wa kuueleza umma wa Tanzania juu ya kilichomsibu Dk. Harrison Mwakyembe.
Najihami mapema kwao kwamba hakuna jambo lolote jipya katika makala hii linaloweza kuwachochea kunifuata; maana yote yalishawekwa wazi kwenye vyombo vingi vya habari, na wala hayakupatwa kukanushwa.
Kwa hiyo, hakuna jipya hapa mbali ya hoja zangu ambazo naamini zinafikirisha. Kama bado watanifuata, basi, lengo lao litakuwa ni kunitisha (mimi na wengine) ili nisiandike tena kuhusu suala hili.
Ndugu zangu, suala ninalojaribu kuliandika kwa tahadhari kubwa hapa ni la masahibu yaliyomkuta Naibu Waziri wa Ujenzi, Mbunge wa Kyela na mmoja wa makamanda wa vita dhidi ya ufisadi nchini, Dk. Harrison Mwakyembe.
Ni karibu miezi miwili sasa tangu Dk. Mwakyembe arejee kutoka India alikopelekwa kwa matibabu ya ugonjwa ambao mpaka sasa umma haujaelezwa rasmi jina lake.
Nimekuwa nikisita kwenda nyumbani kwake kumpa pole, kwa sababu mwenzetu wa Raia Mwema tuliyemtuma kwenda kumuona mara aliporejea kutoka India, alitupa simulizi ya kusikitisha juu ya hali yake. Na mimi kwa udhaifu wa moyo wangu, nahofia ‘presha’ inaweza kunipanda nikimuona, na pengine kuanguka hapo hapo nyumbani kwake.
Kusita kwangu kwenda kumuona na kumpa pole kuliimarishwa zaidi na habari niliyoisoma kwenye gazeti la Tanzania Daima, toleo la Januari 4, 2012, ukurasa wa kwanza, iliyobeba kichwa kinachosomeka “Dk. Mwakyembe ana siri nzito”.
Kwenye habari hiyo ilielezwa kwamba afya ya Mwakyembe inasikitisha; kwani licha ya kupata matibabu nchini India na kuendelea na tiba hiyo hapa nchini, hali yake si ya kuridhisha.
Kwa mujibu wa habari hizo, kucha za vidoleni na miguuni zimeoza na zina rangi nyeusi, miguu na mikono yake imepasuka mithili ya mtu mwenye magamba ambayo wakati mwingine hutoa damu.
Si hivyo tu. Tumeelezwa pia kwamba kichwani hana nywele; kwani zimepukutika zote ikiwa ni pamoja na nyusi za kope. Hali hii humfanya muda wote avae kofia kichwani na glovu mikononi na hata miguuni kuhifadhi viungo vyake hivyo.
Maelezo hayo ya hali ya Dk. Mwakyembe hayanipi mimi, mwenye moyo dhaifu, ujasiri wa kwenda kumuona, na naishia tu kumwombea kwa Mwenyenzi Mungu kwenye sala zangu. Niseme tu kwa Dk. Mwakyembe kupitia makala hii: Hang in there brother, pambana kuokoa maisha yako. Mungu atakusaidia.
Ukweli ni kwamba, kwa yaliyomsibu Dk. Mwakyembe; hata kama atapona kabisa, hawezi kuwa Mwakyembe yule yule tuliyemzoea.
Kwa hakika, atahitaji miaka mingi ya tiba ya kiroho (spiritual healing) na ushauri nasaha kutoka kwa mabingwa wa dunia wa fani hiyo kuweza kusahau yote yaliyomsibu na kuendelea na maisha yake kama kawaida. Huo ndio ukweli wa kipimo cha masahibu yaliyomkuta.
Nikitafakari masahibu hayo yaliyomkuta kamanda huyu wa vita dhidi ya ufisadi, nahisi kuna kitu hakiko sawa katika namna Serikali ya Rais Jakaya Kikwete inavyolishughulikia suala la kiongozi huyo wa Serikali.
Hata hivyo, kabla sijakizungumzia kitu hicho, nianze kwa kumshukuru na kumpongeza Rais Kikwete kwa hatua aliyoichukua ya haraka ya kumpeleka India Dk. Mwakyembe siku alipomtembelea nyumbani kwake na kusononeshwa na hali aliyomkutanayo.
Habari za uhakika nilizonazo ni kwamba Rais Kikwete alihuzunishwa mno na hali ya Dk. Mwakyembe kiasi kwamba alianza hapo hapo sebuleni kwa Mwakyembe kumpigia simu Waziri Magufuli na Waziri wa Afya na kuwapa maelekezo kwamba anataka kuona Dk. Mwakyembe anapelekwa India kwa matibabu ndani ya kipindi cha saa 24! Na ndivyo ilivyokuwa.
Kwa mtazamo wangu; namna Kikwete alivyoishughulikia kwa haraka safari hiyo ya India ya Mwakyembe, ni uthibitisho wa kutosha kwamba Rais wetu ni mwenye huruma na upendo.
Kikwete anaweza akawa na udhaifu wake kiuongozi; lakini ukweli unabaki pale pale kwamba yu mwenye huruma na mpole, na hizo ni sifa zinazotunisha thawabu zake kwa Mungu!
Kuhusu suala la mushkeli ninaouona katika namna ambavyo Serikali yake inavyolishughulikia suala la Mwakyembe, napenda nikite kwenye huu ububu wa Serikali katika kuueleza umma nini hasa kilimsibu jemadari huyo wa vita dhidi ya ufisadi.
Kwa jinsi ninavyofahamu, Dk. Mwakyembe amerejea nchini na ripoti ndefu ya madaktari wa India waliomtibu ambayo inaeleza nini hasa chanzo cha kuzorota kwa hali yake ya afya, na ripoti hiyo ameiwasilisha serikalini; kwani ni Serikali ndiyo iliyompeleka India kwa matibabu. Hili halina ubishi.
Linaloweza kuwa na ubishi lakini unaojadilika, ni hili ambalo nimelijenga katika hisia. Hisia zangu ni kwamba Dk. Mwakyembe mwenyewe anapenda Serikali iweke hadharani ripoti hiyo ya madaktari wake aliyorejeanayo kutoka India. Kwa maneno mengine; Dk. Mwakyembe anataka umma uelezwe nini kilichomsibu.
Baadhi ya watu anaowaamini waliopata kumtembelea nyumbani kwake, si tu amewadokezea kilichomo kwenye ripoti hiyo, lakini pia amesema kwamba kama Serikali itaendelea na ububu wa kutoitoa hadharani, basi, yeye ataeleza umma siri iliyomo kwenye ripoti hiyo ya madaktari wa India.
Sasa kama nipo sahihi kwamba Dk. Mwakyembe mwenyewe anataka umma uelezwe kilichomo kwenye ripoti ya madaktari hao wa India, sielewi ni kwa nini Serikali inasita kufanya hivyo.
Majibu ambayo Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Blandina Nyoni, alilipa gazeti la Majira (toleo hilo la Januari 4); kwamba eti suala la ugonjwa wa Mwakyembe aulizwe mwenyewe Mwakyembe, hayaridhishi na hayana busara ndani yake.
Ni kweli kwamba ugonjwa wa mtu ni siri ya mgonjwa mwenyewe; lakini vipi kama mgonjwa mwenyewe anataka siri ya ugonjwa wake iwekwe hadharani? Na tunao mfano wa ridhaa ya Rais Kikwete kwa daktari wake kuelezea hali ya afya yake (ugonjwa) mbele ya waandishi wa habari. Uamuzi uliofuatia na tukio la yeye (Kikwete) kuanguka jukwaani, mkoani Mwanza.
Isitoshe; hapa hatuzungumzii mgonjwa wa kawaida. Hapa tunazungumzia mgonjwa ambaye ni Naibu Waziri, Mbunge, mwanaharakati wa haki za binadamu na mmoja wa makamanda wa vita dhidi ya ufisadi.
Isitoshe; hapa vilevile tunamzungumzia kiongozi wa ngazi ya waziri ambaye waziri mwingine mwandamizi serikalini, na ambaye ni mpambanaji mwenzake katika vita dhidi ya ufisadi (Samuel Sitta) tayari alishautangazia umma kwamba kinachomsibu Dk. Mwakyembe ni sumu.
Na Samuel Sitta si pekee kuutangazia umma hivyo kwenye kipindi cha Dakika 45 cha ITV; kwani Mwenyekiti wa Halmshauri ya Kyela naye alisema hivyo hivyo na kunukuliwa na magazeti siku alipomtembelea Mwakyembe nyumbani kwake aliporejea kutoka India.
Watu hawa wawili – Sitta na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kyela, ni watu walio karibu sana na Dk. Mwakyembe, na hivyo yawezekana kabisa dhana hiyo ya kupewa “sumu” imetoka kwa Mwakyembe mwenyewe (from the horse’s mouth).
Sasa, kama mazingira ni haya, kwa nini Serikali haioni umuhimu wa kuiweka hadharani ripoti hiyo ya madaktari wa India ili ukweli rasmi ufahamike? Inaona ugumu gani kufanya hivyo?
Kama, kwa mfano, (narudia maneno ‘kwa mfano’ ) kilichomsibu ni kuwekewa sumu ya polonium 210 kama ile iliyotumika kumuua kachero wa Urusi, mjini London, Alexander Litvinenko, basi umma uambiwe; maana katika u-Mafia ambao tumeufikia hivi sasa hapa nchini kwetu, hilo nalo halitatushangaza sana.
Lakini kama pia kilichomsibu si sumu, ni logic (mantiki) umma ukatangaziwa ili fikra hizo kwamba Dk. Mwakyembe aliwekewa sumu ziondoke vichwani mwa Watanzania.
Hivi kuna tatizo gani Waziri wa Afya akaitisha mkutano na waandishi wa habari na akawaeleza, japo kwa ufupi, kilichomo kwenye ripoti hiyo ya madaktari wa India?
Hata kama ripoti inasema kuwa tatizo ni sumu aliyopewa, kuna hatari gani watu kufahamishwa hivyo; hasa kama jeshi la polisi nalo litasema kwamba linaanzisha uchunguzi kujua namna sumu hiyo ilivyompata Mwakyembe?
Nauliza maswali haya yote kwa sababu suala la Mwakyembe si la kawaida, na linaweza kuwa ni tukio la aina yake katika historia ya miaka 50 ya uhuru wetu.
Nasema hivyo kwa sababu, hata kabla hajakumbwa na masahibu haya ya sasa ya mwili kubabuka na kuota magamba; huku nywele na kope zikipukutika, Dk. Mwakyembe alishautangazia umma kwamba maisha yake yamo hatarini.
Huyu ni mbunge na naibu waziri ambaye ataingia katika vitabu vya kumbukumbu kwamba ni mbunge wa kwanza nchini kuandika rasmi barua kwa Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) akilalamika kwamba kuna wauaji wa nje wamekodishwa kuja kumuua, na kisha akatoa maelezo zaidi jinsi walivyomfuatilia kwa gari alipokuwa safarini.
Sikumbuki kama katika historia ya Tanzania ya miaka 50 iliyopita kuna mbunge au waziri aliyemwandikia barua rasmi IGP akimtaarifu kuwa kuna wauaji wa kigeni wanamfuatilia kwa lengo la kumuua. Kama yupo, nikumbusheni.
Lakini japo IGP wetu alikiri kuipokea barua hiyo ya Mwakyembe, hakuna maelezo yaliyotolewa mpaka sasa kama kuna mtu yeyote aliyekamatwa kuhusiana na madai hayo ya Mwakyembe au hata kuuelezea tu umma upelelezi wa suala hilo ulipofikia.
Sasa wakati umma ukisubiri kuelezwa na IGP maendeleo ya uchunguzi wa malalamiko hayo yaliyowasilishwa na Mwakyembe juu ya watu wanaotaka kumuua, ghafla anakumbwa na ugonjwa huo wa ajabu na kukimbizwa India – ugonjwa ambao yeye mwenyewe anaamini chanzo chake ni sumu!
Sasa, katika hali hii, na katika mazingira haya ambapo bado hali ya afya ya Naibu Waziri huyo haijatengemaa; licha ya kupelekwa India kwa matibabu, Serikali haioni lojiki kuiweka sasa hadharani ripoti hiyo ya madaktari wa India waliomtibu ili ukweli ufahamike?
Nionavyo mimi, ni busara Serikali ikatoa tamko sasa kuhusu kilichomsibu Mwakyembe na kuweka hadharani chanzo cha ugonjwa unaomsumbua wakati Mwakyembe mwenyewe angali hai ili awe na fursa ya kukubaliana na hicho kitakachoelezwa na Serikali au kukikataa.
Mungu aepushie mbali, lakini kama Mwakyembe atafariki na kutangulia mbele ya haki, chochote ambacho Serikali itakitamka baada ya yeye kufa kuhusu kilichomuua, hakitaaminika kwa jamii.
Kwa maneno mengine; ni vyema Serikali itamke sasa kuhusu chanzo cha ugonjwa wa Mwakyembe; vinginevyo akifariki, itabidi ifunge mdomo milele!
Nimalizie makala yangu kwa kumwambia tena Dk. Mwakyembe: Hang in there brother, pambana kuokoa maisha yako. Mungu atakusaidia utapona. Watanzania wanakupenda kwa jinsi ulivyojitolea mhanga kuwatetea kwa kupambana na ufisadi.
Kwa upande wa Serikali yetu, nisisitize tena kwamba ina wajibu wa kuueleza umma wa Tanzania juu ya kilichomsibu Dk. Harrison Mwakyembe.

No comments:
Post a Comment