Habari za Punde

*DK. SLAA ATII AMRI YA KUHOJIWA NA POLISI KUHUSU MADAI YAKE KUHUSU VIONGOZI WA CHADEMA KUUNDIWA TRIK ZA KUUAWA

 Katibu Mkuu wa Chadema, Wilbrod Salaa, akiwasili kwenye Ofisi za Makao Makuu ya Jeshi la Polisi jijini Dar es Salaam, leo mchana kutii amri ya polisi iliyomtaka kutoa maelezo kuhusu madai yaliyotolewa na chama hicho  juzi kwamba kuna njama zinafanywa na vyombo vya ulinzi na usalama vya serikali kuwaua baadhi ya viongozi wa chama hicho. Kulia ni aliyekuwa Mbunge wa Arusha mjini, Godbres Lema.
 Askari Poilisi akimuelekeza Dkt. Slaa baada ya kuwasili mahala hapo, ''Haya piteni hapa''.
 Baadhi ya watu waliokuwa Makao Makuu ya Jeshi la Polisi kutaka kujua kilichokuwa kikiendelea.
Dkt. Slaa, akiwasalimia baadhi ya watu waliojitokeza mahala hapo.
 Baadhi ya wafuasi wa Dkt. Slaa, wakilisukuma gari lake wakati likiondoka mahala hapo, baada ya kuhojiwa. Picha kwa hisani ya Habari Mseto.

No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.