Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue, akinyanyua juu mojawapo ya makombe
matano ambayo Ikulu Sports Club, ilinyakua kwenye michezo ya SHIMIWI ya
mwaka huu mjini Dodoma katika hafla ya kukabidhi makombe na kuwazawadia
wafanyakazi bora iliyofanyika jana Ikulu jijini Dar es
salaam. Michuano hiyo ilifanyika kuanzia Septemba 22 hadi Oktoba 10
mwaka huu, ilishirikisha jumla ya wanamichezo 3500 kutoka wizara 56, mikoa 18
na idara za serikali 14 ambapo wanamichezo 91 wa Ikulu walioshiriki walifanikiwa
kuibuka washindi wa kwanza katika michezo ya Baiskeli, Netbal, Kuvuta kamba
wanawake na wanaume na kushika nafasi ya pili ya riadha kwa wanawake na wanaume.
WASHAURI WA WANAFUNZI WATAKIWA KUENDANA NA MABADILIKO YA KIDIJITALI
-
Na Oscar Assenga,TANGA
SERIKALI imekipongeza Chama cha Washauri wa Wanafunzi wa Vyuo Vikuu
Tanzania (TACOGA) kwa kuendelea kuandaa mafunzo yanayole...
9 hours ago


No comments:
Post a Comment