Habari za Punde

*RAIS WA ZANZIBAR DKT. SHEIN ATEMBELEA CHUO CHA WANAWAKE CHA MAFUNZO YA KAZI ZA MIKONO

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akipokea zawadi mara alipowasili katika Chuo cha Mafunzo ya Amali kiitwacho Tilonia,Wilaya ya  Ajmer  Jimbo la Rajastan akiwa  katika siku ya pili ya ziara yake Nchni India pamoja na Ujumbe aliofuatana nao
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akiangalia vifaa mbali mbali katika chuo cha mafunzo ya Amali  kichofundisha wanawake pekee kutoka nchi mbali mbali Duniani ikiwemo Zanzibar,katika cha  Tilonia,Wilaya ya  Ajmer Jimbo la Rajastan akiwa  katika siku ya pili ya ziara yake Nchni India pamoja na Ujumbe aliofuatana nao.
 Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo na Maliasili Affani Othman Maalim (kulia) kwa niaba ta Serikali ya Mapinduzi Zanzibar akitiliana saini makubaliano  ya Uanzishwaji wa Chuo cha Mafunzo ya Amali kwa Wanawake na Chuo cha Barefoot cha India ambapo muanzilishi wa Chuo hicho Bw.Bunker Roy alitia saini (kulia) saini hiyo ilifanyika wakati Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akiwa katika ziara rasmi Nchini India na ujumbe wake.
 Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo na Maliasili Affani Othman Maalim (kulia)   akibadilishana hati za  makubaliano na  Bw.Bunker Roy baada ya kutiliana saini makubaliano  ya Uanzishwaji wa Chuo cha Mafunzo ya Amali kwa Wanawake baina ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na  Chuo cha Barefoot cha India, saini hiyo ilifanyika wakati Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akiwa katika ziara rasmi Nchini India na ujumbe wake katika Eneo la Chuo Kijiji cha Tilonia Wilaya  ya Ajmer Jimbo la Rajastan India.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akibadilishana mawazo na Bw.Bunker Roy Muanzilishi wa Chuo cha Mafunzo ya Amali kwa Wanawake katika Kijiji cha Tilonia  Wilaya ya Ajmer Jimbo la Rajastan pamoja na Balozi wa India Nchini Tanzania  Debnath Shaw (kulia) baada ya Saini ya makubaliano ya uannzishwaji wa Chuo kama hicho Zanzibar.

No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.