Habari za Punde

*MVUA, UPEPO MKALI VYATIBUA MAONESHO YA SIKU YA WANAWAKE MJINI MOROGORO

  Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro, Bi. Theresia Muhongo akisikiliza maelezo kutoka kwa Haji Sajilo ambaye ni Kiongozi msimamizi wa Mipango wa NGO,s ya MOYODEI wakati alipotembelea kwenye mabanda yaliyoharibiwa na mvua iliyoambatana na upepo mkali iliyonyesha jana jioni. Mabanda hayo yalikuwa ni kwa ajili ya maadhimisho ya siku ya Wanawake Duniani iliyokuwa ianze leo jumanne lakini kutokana na maafa hayo maonyesho hayo yamesogezwa mbele hadi tarehe 5/03/2014 kwa ajili ya ukarabati wa mabanda hayo.
 Mkurugenzi wa manispaa ya Morogoro, Bi. Theresia Muhongo akipata maelezo kutoka kwa mama kuhusu mabanda yaliyoezuliwa na mvua iliyokuwa na upepo mkali
 
Baadhi ya Mabanda yakiwa yameharibika vibaya. Picha na Pamoja Geofrey Adroph

No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.