Habari za Punde

*NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI CHARLES KITWANGA AFUNGUA MKUTANO WA BARAZA LA WAFANYAKAZI WA BARAZA LAKE

 Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Charles Kitwanga, akifungua mkutano wa Baraza la wafanyakazi wa Wizara ya Nishati na Madini, uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Hoteli ya Kunduchi Beach jijini Dar es salaam, ulioanza jana na kumalizika leo. Mkutano huo una lengo la kujadili mafanikio na changamoto  katika utendaji  kazi wa Wizara pamoja na taasisi zake.
 Baadhi ya wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi  wa Wizara  ya Nishati na Madini  wakifuatilia kwa makini hotuba iliyokuwa inatolewa na Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Charles Kitwanga (pichani juu).
 Sekretarieti   inayoratibu  mkutano wa baraza la wafanyakazi  la Wizara  ya Nishati  na Madini wakisikiliza kwa makini na kunukuu mada zilizokuwa zinawasilishwa katika mkutano huo.
 Baadhi  ya wajumbe wa baraza la wafanyakazi wa Wizara  ya Nishati na Madini wakiimba wimbo wa kuonyesha mshikamano ujulikanao kwa jina  la “solidarity forever
 Baadhi ya wajumbe  wa baraza la wafanyakazi kutoka Wizara  ya Nishati na  Madini wakifuatilia  kwa makini mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa katika mkutano huo.
 Mwenyekiti  wa Chama cha Wafanyakazi wa  Afya na Serikali Kuu (TUGHE) Wizara  ya Nishati na Madini, Marcelina  Mshumbusi,  akisoma hotuba ya kumkaribisha  Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara  ya Nishati na Madini Mhandisi Ngosi Mwihava  (pichani chini) katika mkutano huo. Kushoto ni Katibu wa TUGHE Wizara ya Nishati na Madini, Assa Mwakilembe.
 Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Mhandisi  Ngosi  Mwihava (kulia)  akisoma hotuba ya kumkaribisha  Naibu  Waziri wa Nishati na Madini, Charles Kitwanga (wa kwanza kushoto). Katikati ni Katibu wa TUGHE Wizara ya Nishati na Madini, Assa Mwakilembe.
 Naibu  Waziri wa Nishati na Madini, Charles Kitwanga (kushoto) akisalimiana na Mhasibu Mkuu Mfawidhi wa Wizara  ya Nishati na Madini, Michael Marandu (kulia) mara baada ya kuwasili kwenye ukumbi wa mikutano ili kufungua mkutano huo.
Naibu  Waziri wa Nishati na Madini Charles Kitwanga  (katikati, waliokaa mbele) na Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara  ya Nishati na Madini, Mhandisi Ngosi Mwihava ( wa pili kutoka kushoto, waliokaa mbele) wakiwa katika picha ya pamoja na  baadhi ya wajumbe wa baraza la wafanyakazi, Wizara ya Nishati na Madini. Picha na Miraji Msala wa Sufianimafoto.com

No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.