Habari za Punde

*KAMATI ZA JUMUIYA NA USULUHISHI WA MIGOGORO KUTEMBELE KAMBI ZA WAKIMBIZI ZA KIGOMA NA RWANDA

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Kufuatia mgogoro wa kisiasa,  jaribio la kumtoa madarakani Raisi  wa Jamhuri ya Burundi, Pierre Nkurunziza na maelfu ya wananchi wa nchi hiyo kukimbilia nchi jirani za Tanzania na Rwanda. 

Hali ya kambi zinazopokea wakimbizi zinaonekana kuelemewa na kupelekea kuhatarisha hali za wakimbizi hao.
Kutokana na hali hiyo, Bunge la Afrika ya Mashariki kupitia kamati yake ya Masuala ya Jumuiya na Usuluhishi wa Migogoro imeteua wajumbe watakao kwenda kutembelea kambi hizi zilizopo Kigoma-Tanzania na Mashariki mwa nchi ya Rwanda kwa madhumuni yafuatayo;
1.     Kujiridhisha na hali ya mazingira ya kambi hizo   na kuangalia mipango ya kutatua mgogoro huo.
2.     Kuangalianakutimizajukumu la Bunge la Afrika Mashariki kupata suluhisho la kudumu la mgogoro ulioko sasa nchini Burundi.

3.     Kuwatemebelea na kuwafariji wananchi wote wa Burundi walioko kwenye kambi hizo.

Wajumbe wa kamati teule wamegawanyika katika makundi mawili, wajumbe watakaokwenda Kigoma-Tanzania wataongozwa naMhe. Abdullah Mwinyi ambae ni mwenyekiti wa kamati hiyo na wajumbe watakaokwenda Mashariki mwa Rwanda wataongozwa naMhe. AbubakarZein.

Imetolewana;
Mhe. Abdullah Mwinyi

(Mwenyekiti  waKamati ya masuala ya Jumuia na Usuluhishi wa Migogoro)

No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.