Kocha msaidizi wa timu ya Taifa 'Taifa Stars, Charles Boniface
Mkwasa, anatarajia kuzungumza na waandishi wa habari kesho kuhusu uteuzi wake
wa kukaimu nafasi ya Kocha Mkuu mkuu wa Stars, huku akirithi, mshahara ule ule
wa sh. milioni 25, gari na nyumba.
Aliyekuwa Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Mart Nooij, aiwa na huzuni wakati akiwa katika mkutano na waandishi wa habari leo,alipokuwa akitangazwa rasmi, msaidizi wake kurithi mikoba yake.
**************************************
Aliyekuwa Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Mart Nooij, aiwa na huzuni wakati akiwa katika mkutano na waandishi wa habari leo,alipokuwa akitangazwa rasmi, msaidizi wake kurithi mikoba yake.
**************************************
AKIZUNGUMZA na waandhishi wa habari jijini Dar es
Salaam, leo mchana, Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Jamal Malinzi
amesema kwamba, kocha mpya wa timu ya taifa, Taifa Stars, Charles Boniface
Mkwasa, atakuwa analipwa kiasi cha fedha kama alichokuwa akilipwa kocha
Mholanzi, Mart Nooij aliyetupiwa virago juzi.
Nooij
aliyekuwa analipwa dola za Kimarekani 12,500 (zaidi ya Sh. Milioni 25) kwa
mwezi, alifukuzwa mwishoni mwa wiki baada ya Taifa Stars kufungwa mabao
3-0 na Uganda Uwanja wa Amaan, Zanzibar.
Katika
Mkutano na Waandishi wa Habari leo, Dar es Salaam, Malinzi amemtangaza
rasmi Mkwasa kuwa kocha mpya wa Taifa Stars akisaidiwa na kocha Hemed
Morocco.
Mkwasa
ambaye ni Kocha Msaidizi wa Yanga na Morocco kocha wa Mafunzo watafanya
kazi kwa kipindi cha miezi mitatu ambayo timu ya taifa itakua na michezo
ya kuwania kufuzu kwa CHAN na AFCON.
Malinzi
amesema uteuzi wa makocha hao wazawa umezingatia vigezo vya makocha wa
timu ya Taifa kuwa na leseni A ya ukocha kutoka CAF au zinazofanana kutoka
mashiriksho mengine duniani wanaozifanyia kazi, jambo ambalo makocha
hao wazawa wamekizi.
“Kocha
Mkwasa atakua akipewa hudumu zote na masilahi (zikiwemo posho) alizokuwa
anapewa kocha aliyeondoka, pia amepewa nafasi ya kuchagua benchi lake la
ufundi la kufanya nalo kazi, hivyo nawaomba wadau wa mpira wa miguu na
watanzania kwa ujumla tuwape sapoti makocha hao wazawa” aliongeza Malinzi”
Aidha
Kamati ya utendaji ya TFF Iimemteua Alhaj Ahmed Mgoyi kuwa mratibu wa timu
ya Taifa, lengo la uteuzi huo wa Mgoyi ni kuwa kiunganishi kati ya kamati ya
Utendaji na timu ya Taifa.

No comments:
Post a Comment