Balozi wa Jamhuri ya Watu wa China nchini Tanzania, Lu
Youqing , akisaini kitabu cha wageni mara baadaya
kuwasili katika Ofisi ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (kulia),
ofisini kwake alipowasili Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa ziara fupi.
Balozi wa Jamhuri ya Watu wa China hapa nchini, Lu Youqin
akizungumza katika kikao na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi. Mhe. Charles
Kitwanga (wa pili upande wa kushoto).
Katika kikao hicho kilichofanyika Wizara hapo, viongozi hawa walijadili
masuala mbalimbali kuhusu ushirikiano wa Serikali ya China na Wizara ya Mambo
ya Ndani ya Nchi.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (kulia),
akizungumza na ujumbe wa Ubalozi wa China nchini Tanzania, ulioongozwa na Balozi LuYouqing,
(hawapo pichani), katika mkutano uliojumuisha pande hizo mbili kuzungumzia
masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya Serikali ya Watu wa China na Wizara
ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (wa nne kutoka
kulia), akiwa katika picha ya pamoja na ujumbe kutoka Ubalozi wa China nchini
Tanzania, ulioongozwa na Balozi Lu Youqing (watatu kutoka kulia). Ujumbe huo
ulitembelea Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kujadili masuala mbalimbali kuhusu
ushirikiano kati ya Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China na Wizara ya Mambo ya
Ndani ya Nchi. PICHA
NA KITENGO CHA MAWASILIANO YA SERIKALI – WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
No comments:
Post a Comment