Habari za Punde

*ASKARI WA KIKE WA MAKETE ABAKWA


Watu wasiofahamika wakazi wa wilaya ya Makete mkoani Iringa wamembaka na kumlawiti vibaya askari mmoja wa Kike (jina limehifadhiwa) baada ya kunywa pombe kupita kiasi .

Tukio hilo liletoka jana katika bar ya V.I.P iliyopo mjini Makete ambapo vyanzo vya habari hii vinadai kuwa askari huyo ambaye awali kabla ya kuhamishiwa wilaya ya makete alikuwa mjini Iringa kikazi ,kuwa alikuwa akinywa pombe na mshikaji wake wa siku zote ambaye ni mfanyabiashara wa Tunduma mkoani Mbeya aliyefika wilaya ya makete kwa ajili ya kesi iliyokuwa ikimkabili. 



Imedaiwa kuwa baada ya wawili hao kunywa pombe zaidi ya kreti moja wawili ghafla vijana wa kihuni walimwita nje njemba huyo na kumpa kipigo cha nguvu na wakati akielekea polisi kushtaki nyuma askari huyo W.P alitoka nje ya bar hiyo akiwa amelewa na kwenda kujisaidia nyuma ya bar hiyo ambako alikutana na mkasa huo wa kufanyiwa kitu mbaya. Hata hivyo W.P huyo alikutwa na wasamaria wema akiwa amezidiwa kuwa kubakwa huku wakiwa wamempakaza kinyesi ambacho alikuwa ameachia wakati akiwa amebakwa, hadi sasa amelazwa katika hospitali ya wilaya ya makete Ikonda. Na Francis Godwin, Iringa

No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.