Habari za Punde

*YANGA KIDUME KOMBE LA KAGAME YAICHAPA SIMBA 1-0

 Wachezaji wa Yanga ya Dar es Salaam, wakishangilia ushindi na Komne lao baada ya kukabidhiwa kombe hilo kwa kuibuka kidedea baada ya kuwafunga watani wao wa jadi Simba kwa bao 1-0, katika mchezo wa fainali ya Kombe la Kagame uliochezwa leo jioni kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Bao hilo lilifungwa na Asamoh baada ya krosi murua kutoka kwa Rashid Gumbo aliyemtoka Ulimboka mwakingwe katika dakika za nyongeza baada ya kumalizika dakika 90 bila kufungana.
 Ubao ulisomeka hivi hadi mwisho wa mchezo huo.
 Kipa wa Simba Juma Kaseja, akiruka kuokoa mpira bila mafanikio uliopigwa na Asamoh kwa kichwa na kuandika bao la kwanza na la ushindi kwa Yanga.
 Liziwani Kikwete (kulia) akishangilia ushindi wa Yanga na shabiki mwenzake, Muddy Sebene, baada ya mchezo huo kumalizika.
Hekaheka langoni mwa Simba.

No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.