Habari za Punde

*TFF YATAJA KIINGILIO MECHI YA YANGA NA SIMBA NI BUKU 5


 Kiingilio cha chini kwenye mechi ya Yanga na Simba itakayochezwa Jumatano (Oktoba 3 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kitakuwa sh. 5,000 kwa viti vya rangi ya kijani ambavyo ni 19,648 kwenye uwanja huo wenye uwezo wa kuchukua watazamaji 60,000.
Mechi hiyo namba 80 ya Ligi Kuu ya Vodacom itachezwa kwenye uwanja huo kuanzia saa 11 kamili jioni. Watazamaji watakaotaka kuona mechi hiyo wakiwa wameketi kwenye viti vya rangi ya bluu ambavyo ni 17,045 watalipa sh. 7,000 kwa tiketi moja.
Viingilio vingine kwenye mechi hiyo ni sh. 10,000 kwa viti vya rangi ya chungwa ambavyo viko 11,897 wakati VIP C inayochukua watazamaji 4,060 itakuwa sh. 15,000. Kwa upande wa VIP B tiketi ni sh. 20,000 na VIP A yenye watazamaji 748 tu kiingilio kitakuwa sh. 30,000.
SIMBA vs TANZANIA PRISONS LINE UPS
Timu za Simba na Tanzania Prisons zinapambana jioni hii Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 11 kamili jioni. Tayari makocha wa timu zote mbili Jumanne Charles (Tanzania Prisons) na Circo Milovan (Simba) wameshataja vikosi vyao.
Simba:                                                  Tanzania Prisons:
01.Juma Kaseja (c)                            18.David Abdallah
02.Nassoro Masoud                             03.Aziz Sibo
17.Amir Maftah                                  05.Laurian Mpalile
15.Shomari Kapombe                          16.Lugano Mwangama (c)
24.Juma Nyoso                                   15.David Mwantika
14.Mwinyi Kazimoto                            13.Khalid Fupi
28.Amri Kiemba                                  07.Misango Magai
08.Ramadhan Chombo                         12.Fred Chudu
19.Edward Christopher                        14.Elias Maguri
10.Felix Sunzu                                     17.Peter Michael
16.Mrisho Ngasa                                   19.John Matei
Wachezaji wa akiba;
22.Wilbert Mweta                                 01.Daudi Mwasongwe
23.Paul Ngalema                                   04.Jumanne Elfadhili
20.Jonas Mkude                                     09.Sino Augustino
12.Salim Kinje                                       22.Julius Kwaga
04.Komanbil Keita                                 08.Henry Mwalugala
13.Daniel Akuffor                                   11.Hamisi Ally
05.Pascal Ochieng                                  23.Jeremiah Juma
Refa: Paul Soleji (Mwanza)
Mwamuzi Msaidizi 1: Jesse Erasmo (Morogoro)
Mwamuzi Msaidizi 2: Mwarabu Mumba (Morogoro)
Mwamuzi wa Akiba: Israel Nkongo (Dar es Salaam  

No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.