Habari za Punde

*BALOZI IDDI AKAGUA JENGO LA SKULI YA SEKONDARI YA DONGE

 Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi pamoja na Mbunge wa Jimbo la Donge kulia yeke Mh. Sadifa Juma Khamis, Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja Kanal Mstaafu Juma Kassim Tindwa kushoto ya Balozi Seif  wakilikagua jengo la skuli ya sekondari la Donge ambalo limeanza kutua huduma. Wa kwanza kulia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi wa Jumuiya ya Maendeleo Donge Maalim Khamis Mohamed.
 Jengo la Ghorofa mbili la Skuli ya Sekondari ya Donge Mkoa wa Kaskazini Unguja ambalo tayari limeanza kuhudumia wanafunzi wa Sekondari baada ya kukamilika kwa hatua ya uezekaji.
Baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Uongozi wa Jumuiya ya Maendeleo Donge wakifuatilia hotuba ya kuzinduliwa  kwa Jumuiya hiyo kulikofanywa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi hayupo pichani. Picha na Hassan Issa wa –OMPR – ZNZ.
*********************************************************

No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.