Habari za Punde

*KILELE CHA MAADHIMISHO YA 18 YA WIKI YA MAZIWA KITAIFA BABATI,MANYARA

 Skauti wakimkalibisha skafu, Waziri wa Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi Dkt. Kiete Kamani, wakati alipowasili kuhudhuria sherehe za Kilele cha Maadhimisho ya 18 ya Wiki ya Maziwa Kitaifa Wilaya ya Babati -Manyara, jana

Mwenyekiti wa Bodi ya Maziwa Dr, Aichi Kitalyi akiwakaribisha wageni waalikwa katika Kilele cha Wiki ya Maadhimisho ya 18 ya Wiki ya Maziwa Kitaifa katika viwanja vya Kwaraha Babati -Manyara.
Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mh Joeli Bendela,  akimkalibisha Waziri wa  Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi Dkt. Titus Kamani, Kuhutubia katika Maadhimisho ya 18 ya Wiki ya Maziwa Kitaifa Mkoani Manyara.  

Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi Dkt. Titus Kamani, akihutubia wakati wa sherehe za Kilele cha Maadhimisho ya 18 ya Wiki ya Maziwa Kitaifa Mkoani Manyara, 
***********************************
Akihutubia katika sherehe hizo, Kamani, alisema kuwa anaamini kuwa ni Fulsa Nzuri kwa Wafugaji na wakazi wa Mkoa wa Manyara, kwa ujumla kwa kuweza kuona na Kujifuza jinsi ya Kuzalisha aina ya Mbegu nzuri  ya  Ng'ombe ambao wakifugwa kitaalamu, wataongeza upatikanaji wa lita nyingi za Maziwa.

''Na kuongezeka kwa upatikanaji wa lita nyingi za maziwa pia kutaongeza kipato kwa kilamwananchi na Uchumi Kwa Taifa''. alisema

Kamani aliwataka wafugaji kuongeza juhudi katika sekta hiyo ya ufugaji, baada ya kuona maendeleo yatokanayo na bidhaa hiyo, na mapungufu katika eneo la usindikaji.

Aidha, Kamani, aliwashukuru wadhamini wanaotoa huduma za Kibenki kwa wafugaji kama CRDB, NMB na Exim Benk kwa Kuingia katika Sekte Hiy ili Kuwasaidia Wafugajia na Wasindikaji Katika Kuwapatia Mikopo Iliyokua nafuuu zaidi, Kauli Mbiu ya Kilele hicho ilikuwa ni 'Ng;ombe wa Maziwa  ni Fulsa ya Kiuchumi na Lishe'.
Baadhi ya Wananchi wa Mkoa wa Manyara wakimsiiliza Waziri
Kikundi Cha Masai wakitoa Burudani 
Pia wafugaji walitoa shoo yao ya Gwaride la Ng'ombe kwa kuwapitisha mbele ya Mgeni rasmi.
Baadhi ya wanafunzi wa Shule mbalimbali na walimu wao wakipozi kwa picha na Tuzo zao walizokabidhiwa na Waziri huyo.
Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi Dkt. Titus Kamani, akitembelea baadhi ya mabanda katika kilele hicho. Picha na Miraji Msala.

No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.