Habari za Punde

*MWANDISHI, MICHAEL MACHELLAH AJITOSA KUWANIA UDIWANI KATA YA MAKUMBUSHO

Na Mwandishi Wetu, Dar
MWANAHABARI Michael Shija Machellah aliyewahi kufanya kazi katika Kampuniya New Habari 2006 Ltd,  inayozalisha Magazeti ya Mtanzania, Rai, The African, Bingwa na Dimba na baadaye Business Times na Majira amejitosa kwenye mbio za kuwania Udiwani Kata ya Makumbusho jijini Dar es Salaam kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Akizungumzi uamuzi wake huo, Machellah, alisema ameamua kutia nia ya kuwania kiti hicho baada ya kujitafakari kwa kina mwenyewe kutoka moyoni akiwa na nia thabiti ya kuleta mabadiliko ya kimaendeleo katika eneo analoishi endapo Chama CHA CCM kitampa ridhaa ya kugombea eneo hilo na kuking’oa Chama cha CUF, kinachoshikilia kiti hicho.

Alisema Machellah yeye nimzaliwa wa Mwananyamala, Kata ya Makumbusho na anaishi Kata hiyo jijini Dar es Salaam hivyo ana kila sababu ya uzalendo wa kutia nia kwa maana halisi ya kutaka mabadiliko katika Kata yake kupitia CCM.

Machellah alizaliwatarehe 19/08/1975 Katika Hospitali ya Ocean Road jijini Dar es Saalam, alipata elimu ya Msingi Kijijini kwa Wazazi wake Mwime Kahama Mkoani Shinyanga, Alipata Elimu ya Secondari katika Seminari ya Mt.Joseph Ujiji Mkoani Kigoma na ana Diploma ya taaluma ya Uandishi wa Habari ambayo aliipata jijini Dar es Salaam katika Chuo cha Dar es Salaam School of Journalism (DSJ).
Machellah kwa sasa ni Mwajiliwa katika Kampuniya Integrated Communications Limited kama Afisa habari katika kitengo cha Mawasiliano na mahusiano (PR) cha moja ya vitengo vya Kampunihiyo.


Wito kwa wakazi wa Kata ya Makumbusho kwa mwaka huu wa uchaguzi wasifanye makosa waliyolifanya awamu iliyopita jiandae vyema kukirudisha Chama cha Mapinduzi Madarakani katika Kata yako na zaidi Mchague Michael Machellah (NGOSHA) kwa maendeleo ya Kata yako ya Makumbusho.  

No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.