Habari za Punde

*UP DATE KUTOKA WHITE HOUSE DODOMA USIKU HUU, KIKAO CHA KAMATI KUU CHAPITISHA MAJINA MATANO, KUTAJWA KESHO, WAJUMBE WA3 WATANGAZA KUGOMEA MATOKEO

 Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, akizungumza na waandishi wa habari nje ya ukumbi wa mikutano wa CCM Makao Makuu mjini Dodoma usiku huu baada ya kumalizika kwa Kikao cha Kamati Kuu kilichoanza mchana wa leo, ambapo amesema kuwa Kamati imemaliza kazi yake ya kupitisha jumla ya majina matano ambayo yatatajwa kesho saa nne asubuhi kabla ya kuingika katika kikao cha kesho.
 Wakati Nape akitangaza taarifa hiyo naye Mjumbe wa Kamati Kuu, John Nchimbi, alitoka nje ya lango hilo na kutoa tangazo kuwa wanahabari wasiondoke kwamba wasubiri baada ya dakika ishirini atakuja kuzungumza nao, na ndipo alipomaliza Nape na Nchimbi aliwakusanya  wanahabi na kusema kuwa Yeye na wenzake watatu, wamegomea matokeo hayo na kutangaza kujitoa rasmi ujumbe wa Kamati hiyo.

Nchimbi, aliwataja wajumbe hao kuwa ni pamoja na Sophia Simba, Adam Kimbisa na yeye mwenyewe.

"Kwa hiyo sisi watatu tunatangaza kutoyaunga mkono matokeo hayo na tanajitenga na matokeo hayo'', alisema Nchimbi.
 Nchimbi, akiwatangazia wanahabari kuwataka wasiondoke eneo la tukio na badala yake kuwataka wasubiri baada ya dakika 20 ili arudi kuwatangazia maamuzi ya wajumbe wenzake walioafikia kugomea matokeo.
 Wengine walikuwa wakitoka wamenuana na wengine wakiwa wamefurahi, kama anavyoonekana Lukuvi akitabasamu huku akionyesha ishala ya Dole kuwa mambo ni poa.
 Wanahabari wakisubiri kupata matokeo usiku huu kabla ya Nape kutoka na kutangaza kuwa majina hayo yatatangazwa kesho majira ya ssa nne asubuhi.
 Wanahabari wakisubiri kupata matokeo usiku huu kabla ya Nape kutoka na kutangaza kuwa majina hayo yatatangazwa kesho majira ya ssa nne asubuhi.

No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.