Kituo cha Uwekezaji
Tanzania (TIC) kimethibitisha Tanzania kupokea uwekezaji mkubwa wenye thamani
ya Dola za Marekani milioni 100, ambao utachangia kwa kiasi kikubwa sana katika sekta ya utalii na uhifadhi maliasili nchini. Hati
ya Uwekezaji Mkubwa wa Kimkakati imetolewa kwa mradi huo mwanzoni mwa Septemba 2015 na Kamati ya
Taifa ya Uwekezaji wa Kimkakti, (NISC) iliyoko chini ya Uenyekiti wa Waziri
Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mizengo Peter Pinda (MB).
Uwekezaji huo anatoka nchini Marekani na ni matokeo ya moja kwa moja ya juhudi
zinazofanywa na Mheshimiwa Rais Dr. Jakaya Mrisho Kikwete na Serikali yake kwa
juhudi kubwa za kuitangaza Tanzania ndani na nje ya nchi, hivyo kubutia
uwekezaji katika sekta ya Utalii hivyo kukukuza sekta hiyo kwa uwekezaji wa
moja kwa moja kutoka nchi za nje.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania, TIC, Bi Juliet Kairuki alisema kuwa
"Kituo chake kimefurahishwa na nia ya dhadi ya uwekezji mkubwa, ilioonyeshwa
na mwekezaji wa kutoka nchini Marekani
(Taasisi ya Friedkins Family (FCF)) ambapo ni kuitikia mwito wa serikali ya
Tanzania kukaribisha uwekezaji wa ndani na nje ya nchini ambayo ndio injini ya
uchumi wa taifa,.
Bibi Kairuki amesema "Huu ni Uwekezaji Mkubwa wa Kimkakati wa
pili katika sekta ya Utalii katika kipindi cha miaka mitatu ambao umechangiwa
na juhudi na kazi nzuri iliyofanywa na Waziri
wa Maliasili na Utalii, Mhe. Lazaro Nyalandu na timu yake katika Wizara ya
Maliasili na Utalii, na tunamatumaini kazi hii nzuri ya kulrta wawekezaji
wakubwa, katika sekta ya utalii nchini itaendelea "

Uwekezaji huu utazalisha, ajira mpya, uhifadhi wa wanyamapori, maendeleo ya
utalii, maendeleo ya jamii za vijijini, maendeleo ya miundombinu, na maendeleo
katika maeneo ambayo kwa sasa kuvutia idadi ya ndogo ya watalii kama Kanda ya
Magharibi ambapo kuna uhaba wa wanyamapori, uwekezaji huu unatarajia kuanzisha
utalii wa picha na na utalii wa
utamaduni kama njia ya kuvutia watalii katika
maeneo haya.
Mbali na kuwekeza, FCF itafanya kazi kwa karibu na Idara ya Wanyamapori ya
Tanzania, katika Wizara ya Maliasili na Utalii juu ya mipango ya kupambana na
ujangili na itaendelea kudhamini na kusimamia uendeshaji wa Mfumo wa Taarifa za
Kijiografia (GIS) katika kusaidia juhudi za kupambana na ujangili.
Kati ya mwaka 2005 na 2015 TIC imesajili miradi ya utalii 1856. Kati ya hii,
miradi 1150 ni ya wawekezaji wa ndani, 324 wawekezaji wa nje na 382 ni ya ubia
kati ya wawekezaji wa nje na wenyeji. Miradi hii inatarajiwa kuzalisha ajira
zaidi ya 97,000 na kuzalisha mapato ya zaidi ya dola milioni 6,913.24 za Marekani katika
uwekezaji.
MWISHO.
Imetolewa na TIC
Taarifa kwa wahariri.
Kituo
cha Uwekezaji Tanzania (TIC) ilianzishwa mwaka 1997 na Sheria ya
Uwekezaji Tanzania kuwa "Shirika la Msingi la Serikali kuratibu,
kuhamasisha, kukuza na kuwezesha uwekezaji katika Tanzania na kuishauri Serikali
juu ya sera ya uwekezaji na masuala yanayohusiana."
Mikataba
shirika na miradi yote ambao kiwango cha chini uwekezaji si chini ya Marekani $
500,000 kama kigeni inayomilikiwa au Marekani $ 100,000 kama ndani ya nchi
inayomilikiwa. Makampuni ya kushiriki katika uchimbaji wa madini na mafuta ya
petroli zitafuatana mchakato wa kupitishwa zilizomo katika sheria zao. Hata
hivyo, shirika watawasaidia wawekezaji wote kupata vibali, idhini nk
inavyotakiwa na sheria nyingine ili kuanzisha na kuendesha uwekezaji nchini
Tanzania.
Kamati
ya Uendeshaji Uwekezaji Taifa
Katika
jitihada za kuboresha mazingira ya biashara na kukuza uchumi kupitia kuongezeka
kwa uwekezaji, Serikali sumu Taifa Uwekezaji Kamati ya Uendeshaji chini ya
uenyekiti wa Mhe. Waziri Mkuu.
Wajumbe
wengine wa kamati ni Waziri wa Fedha, Waziri wa Viwanda na Biashara, Waziri wa
Kilimo, Waziri wa Ardhi, Waziri wa Uwekezaji na Uwezeshaji, Mwanasheria Mkuu wa
Serikali, Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania na Mkurugenzi Mtendaji wa TIC
(Katibu).
Kamati
hii ni waliokabidhiwa na wajibu wa uundaji wa sera za uwekezaji na kutatua
matatizo ya wawekezaji juu ya kufunga kufuatilia msingi.
Hadi sasa, serikali, kupitia NISC, ina kibali 41
Mkakati wa Uwekezaji Miradi ambayo 12 ni miradi ya kilimo

No comments:
Post a Comment