Rais Mstaafu wa Jamahuri ya Muungano Tanzania na Mwenyekiti wa CCM Taifa Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete(kulia) akisisitiza jambo wakati alipofuatana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli kabla ya kuingia katika ukumbi kikao cha siku moja cha Kamati Kuu ya Chama cha Mapinduzi CCM kilichofanyika leo Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma.
Baadhi ya Wajumbe wa Kikao cha Kamati Kuu ya CCM wakiwa katika Ukumbi wa Mkutano uliofanyika leo chini ya Mwenyekiti wake Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe,Mjaliwa Kassim Majaliwa (kulia) akiwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar,akifutatiwa na Waziri Mkuu Mstaafu Salim Ahmed Salim na Dkt.Bi Mauwa Daftari wakiwa katika kikao cha siku moja cha Kamati Kuu ya CCM uliofanyika leo katika ukumbi wa Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma,chini ya Mwenyekiti wake Rais Msataafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan akiwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Nd,Majaliwa Kassim Majaliwa wakati wa Mkutano wa siku moja wa Kamati Kuu ya CCM uliofanyika leo katika ukumbi wa Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma na kuongozwa na Mwenyekiti wake Rais Msataafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete.
Rais Mstaafu wa Jamahuri ya Muungano Tanzania na Mwenyekiti wa CCM Taifa Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete(katikati) akiongoza kikao cha siku moja cha Kamati Kuu ya CCM kilichofanyika leo katika ukumbi wa Ikulu Chamwino Mkoa wa Dodoma, (kushoto) Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohmed Shein,(kulia)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan akibadilishana mawazo na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohmed Shein,(kulia) baada ya kumalizika kikao cha siku moja cha Kamati Kuu ya Chama cha Mapinduzi CCM kilichofanyika leo Ikulu ya Chamwini Mkoani Dodoma. Picha na Ikulu.






No comments:
Post a Comment