Habari za Punde

*MAKHILIKHILI WATUA DAR KUFANYA MAONYESHO TANZANIA BARA NA VISIWANI


Baadhi ya Wasanii wanaounda kundi la Makhilikhili, wakionyesha vionjo vyao wakati wa mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo mchana, kuhusiana na maonyesho yao wanayotarajia kufanya hapa nchini, baada ya kuwasili jana. Kiongozi wa kundi hilo la Dansi ya asili kutoka Botswana la Makhilikhili, Moses Malapela ‘Shumba Ratshega’, aliyefika nchini na kundi lake kwa ajili ya maonyesho kadhaa, alitoa tafsiri ta neno MAKHILIKHILI kuwa ni mwanaume ama mwanamke anayetoka nje ya ndoa yake yaani kuisaliti ndoa na kupenda kufanya mapenzi nje ya ndoa yake, ambapo alisema kuwa neno hilo kwa nchini kwao linatumika kikawaida kabisa japo linaoshesha kuwa ni 'matusi' lakini linatumika namna hiyo ili kuweza kufikisha ujumbe kutokana na hali mbaya ya maambukizi ya Ukimwi nchini kwao. Tigo ni miongoni mwa wadhamini wa ujio wa kundi hilo.
Wasanii wa kundi hilo wakiingia katika ofisi za Tigo kwa ajili ya mahojiano na waandishi wa habari leo mchana.

Makhilikhili, wakiingia kwa mapozi Tigo.

Kiongozi wa kundi la Dansi ya asili kutoka Botswana la Makhilikhili, Moses Malapela ‘Shumba Ratshega’, akifafanua juu ya jina wanalotumia na maana yake wakati akizungumza na waandishi wa habari leo (wapili kushoto) ni mratibu wa kundi hilo, Scholastica Muzula, Ofisa Uhusiano wa Tigo, Jackson Mmbando na Ofisa Viwango wa Tigo, David Zacharia.


No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.