UONGOZI mpya wa Mabingwa wa soka Tanzania Bara, timu ya Simba ya jijini Dar es Salaam leo umekabidhiwa rasmi nyaraka za ofisi pamoja na
Makabidhiano hayo yaliyofanyika kwenye Makao Makuu ya klabu hiyo yaliyopo mtaa wa Msimbazi Kariakoo, ilionekana kuwapo kwa dosari kwa uongozi wa klabu hiyo chini ya Mwenyekiti Hassan Dalali kushindwa kukabidhi hati ya majengo mawili ya klabu hiyo.
Katibu Mkuu wa klabu hiyo Mwina Kaduguda, alisema kuwa hati hizo wameshindwa kukabidhi kwa uongozi mpya kwa kuwa hati ya jengo jipya ipo mikononi mwa mpangaji Haji Salim Hemed, ambaye mkataba wake unamalizika mwaka 2014, wakati ile ya jengo la zamani anayo Mjumbe wa Baraza la Wazee wa klabu hiyo Hamisi Kilomoni.
Makabidhiano mengine yaliyofanyika ni pamoja na mkataba wa timu hiyo na Kampuni ya Bia Tanzania [TBL], mkataba wa Push Mobile, Katiba ya Klabu hiyo, Akaunti tatu za Benki, mabasi mawili yaliyotolewa na TBL, Coaster yenye namba za usajili T 677 AZR, T 688 AZU na lile ambalo lilikuwa kwa ajili ya kocha, T 229 AUF lililopo yadi na ule mkataba wa kampuni ya Kimarekani ya Snejjer Sports and Casual Wear amabo utaiwezesha timu hiyo kupatiwa vifaa vya michezo kwa mwaka mzima na Kombe la Ubingwa wa Ligi Kuu.
Katika hatua nyingine, Katibu huyo, Kaduguda aliwataka viongozi wa klabu hiyo chini ya Mwenyekiti wake Ismail Aden Rage, Makamu wake Gofrey Nyange ambao wameingia madarakani baada ya uchaguzi mkuu uliofanyika Mei 9 mwaka huu kujali maslahi ya timu na kuendeleza umoja na mshikamano ili amani itawale ndani ya klabu na kuifanya iwe na mafanikio zaidi.
Naye Mwenyekiti aliyemaliza muda wake, Dalali alitumia fursa hiyo kuwapongeza wachezaji kwa ushindi wa mabao 2-1 jana dhidi ya Atraco katika Mashindano ya Kombe la Kagame yanayoendea nchini
“Nashukuru na kuwapongeza sana vijana na wahakikishe kuwa Kombe hilo linakuja nyumabani, lakini leo tunaweka msingi wa kihistoria wa kukabidhiana ofisi na mali za klabu kwa amani na kwa mara ya kwanza tangu kuanzishwa kwa Klabu hii, naamini tukiendeleza umoja huu Simba itakuwa ya kisasa zaidi”, alisema.
Naye Rage alimpongeza Dalali kwa kuonyesha kitendo cha uungwana kwa kukabidhi ofisi na kusema kuwa hiyo ni dalili ya uadilifu.
“Kanuni ya 29 ya FIFA (Shirikisho la Soka Duniani) inazungumzia uadilifu na hata wenzetu wa nyumbani (Shirikisho la Soka Tanzania TFF) wanasisitiza juu ya
No comments:
Post a Comment