Habari za Punde

*WANACHAMA CUF WAMCHANGIA 500, 000 LIPUMBA KUCHUKUA FOMU YA URAIS

Mwenyekiti wa Chama cha CUF, Profesa Ibrahim Lipumba (kushoto) akikabidhiwa fomu ya kugombe nafasi ya Urais na Katibu wa Chama hicho wa Wilaya ya Kinondoni Dar es Salaam, Kassim Chogamawano, wakati wa hafla hiyo iliyofanyika leo mchana kwenye Ofisi ya Chama hicho Tawi wa Mnazi Mageuzi iliyopo Temeke jijini. Katikati ni Mwenyekiti wa Chama hicho, Wilaya ya Kinondoni, Juma Nkumbi.

Profesa. Lipumba akifurahia fomu yake baada ya kukabidhiwa.

Prof. Lipumba akisalimiana na Mzee wa Chama hicho kwa bashasha na furaha za hali ya juu wakati alipofika kuchukua fomu hiyo.

Mwenyekiti na Katibu, wakikagua Kadi ya Uanachama ya Prof. Lipumba kabla ya kumkabidhi Fomu.

Baada ya kukaguliwa furaha ya mzee huyo ilirejea tena kwani aliruka na kumkumbatia huku wakifurahi kwa pamoja na kufanya umati wa wanachama lukuki waliokuwapo mahala hapo kuangua kicheko cha furaha na vigelegele.

Hawa ni sehemu tu ya Wanachama wa CUF, waliokusanyika nje ya ofisi ya Chama hicho Temeke, kumshuhudia mwenyekiti wao akikabidhiwa fomu ya kugombea nafasi ya urais katika uchaguzi mkuu ujao.

Hapa ni wakati Lipumba akipokelewa kuingia kwenye Ofisi za Chama hicho.

Hapa ni wakati Mwenyekiti wa Chama hicho Tawi la Mnazi Mageuzi, Azizi Ngamwembe (kushoto) akimkabidhi kitita cha fedha Sh. 500,000, zilizochangwa na wanachama, kwa ajili ya kumsaidia kulipia Fomu ya kuwania nafasi ya urais.

Prof. Lipumba, akiwasalimia Wanachama wake waliokuwapo eneo hilo wakisubiri kushuhudia zoezi hilo la kukabidhiwa fedha na fomu.

Katika hafla hiyo, Burudani nazo hazikiwa nyuma, hiki ni kikundi cha Sanaa na wanachama wakisebeneka miondoko ya ngoma za kizaramo....

Hawani ni baadhi ya wanachama, wakiimba nyimbo za Chama hicho wakati wakisubiri kumpokea Mwenyekiti wao.

Ebwana eeeh! Kiduku cha huyu mzee usipime, kwani alikuwa akimwaga kiduku cha kufa mtua na cha aina yake na kuwaacha hoi watu waliokuwapo maeneo hayo.....Hebu mcheki katika picha zijazo staili tofauti tofauti...

Hapoo Hapooo Hapo sasaaaaaaaaaa!

Hili Sebene lilikuwa la kukata na shoka.......














No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.