Habari za Punde

DK. BILAL AINGIA MKOA WA MTWARA AUNGURUMA KWENYE UWANJA WA MASHUJA

Baada ya kumaliza ziara yake ya mkoa wa Lindi katika kuinadi Ilani ya Chama cha Mapinduzi, hatimaye Mgombea Mwenza Dk. Mohamed Gharib Bilal, leo jioni amepokelewa kwa shangwe kubwa na wananchi wa Mkoa wa Mtwara na kuanza kuwahutubia wananchi hao katika mkutano wake wa kwanza katika mkoa huo kwenye Uwanja vya Mashujaa. Dk Bilal kesho anatarajia kuanza safari ya kuelekea Vijiji vya Mkoa huo kwa ajili ya kuinadi Ilani na kumuombea Kura Mgombea Urais Dk Jakaya Kikwete, Wabunge na Madiwani wanaowania nafasi hizo kupitia tiketi ya Chama cha Mapinduzi.

No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.