Mfanyabiashara wa nyanya akizoa nyanya zake zilizomwagika katikati ya Barabara eneo ya Amana Dar es Salaam leo mchana. Pamoja na kuona Roli likija mbele yake kwa kasi huku likifunga breki na kuliza Mbwa, lakini bado kijana huyo hakuthubutu kusogea pembeni kulipisha aliendelea tu na zoezi lake la kuzoa nyanya zake hadi rili lilipoamua kusimama na kumkepa huku watu waliokuwapo eneo hilo pembeni mwa Barabara hiyo, wakimpigia kelele kumuashiria aziache nyanya hizo ili kuokoa maisha yake.
TCRA na TAMWA wamekuja na hii kwa waandishi wa habari
-
Leo 24 Oktoba 2024 – Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania
(TAMWA), kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA),
wamezungumza na...
1 hour ago
No comments:
Post a Comment