Baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Msingi Mzambarauni Gongolamboto, jijini Dar es Salaam, wakiwa nje ya madarasa yao baada ya kuwasili shuleni hapo leo kwa mara ya kwanza tangu ilipotokea milipuko ya mabomu katika Kambi ya 511 KJ ya Jeshi la Wananchi (JWTZ) wiki iliyopita. Mahudhurio ya wanafunzi hao yamepungua tofauti na awali kutokana na hofu ya milipuko hiyo. Imeelezwa kuwa hapo awali Darasa moja lilikuwa na watoto 80, lakini leo kila darasa watoto walioripoti hawafikii hata 40, na hii inawezekana ni kwasababu ya hofu ya wazazi ambapo wengine wameamua kuwasafirisha watoto wao mikoani amba kuwahamisha shule na pengine kati ya watoto ambao hawajapatikana hadi hii leo ni miongoni mwao.
MAKAMU WA RAIS AFUNGUA MKUTANO WA MAAFISA WAANDAMIZI WA MAGEREZA
-
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango
akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Hamad Masauni wakati
alip...
1 minute ago
No comments:
Post a Comment