Msanii wa maigizo, Mzee Small (katikati) akimkabidhi Tuzo Man Water, kwa niaba ya 20 Pacent, aliyeibuka kidedea katika Kategoli ya Wimbo bora wa Afro Pop, (kulia) ni Bi Chau. Msanii huyo jana katika onyesho la kutoa tuzo hizo za 'Tanzania Kili Music Awards' alifunika na kuweza kujizolea jumla ya tuzo tano na kuufanya ukumbi kuzizima kwa makelele ya kushangilia kila alipotajwa jina kushiriki katika Kategoli fulani. Hata hivyo msanii huyo hakuweza kuhudhulia onyesho hilo kutokana na kupata safari ya ghafla kulingana na maelezo ya mwakilishi wake, ambaye pia ni Producer wake Man Water. Mashabiki waliohudhulia onyesho hilo, wakishangilia baada ya kutajwa jina la 20 Pacent.
Jay Moe (wapili kushoto) JBC na Producer, wakipozi na tuzo zao baada ya kutwaa tuzo hizo jana usiku.
Khalid Chokoraa (kulia) akipokea tuzo yake ya kuwa rapa bora wa mwaka.
Mchezaji wa timu ya Yanga, Jerry Tegete (kulia) akimkabidhi tuzo ya Wimbo bora wa Raggae Dance hall, msanii C-Pwaa. Kushoto ni mchezaji wa Simba, Mussa Hassan 'Mgosi'.
Mashabiki wakipata raha ukumbini humo.
Raha zinaendelea ukumbini, mashabiki wakifuatilia kwa makini kila linalofanyika jukwaani.
Mwenyekiti wa Kamati ya ushindi ya timu ya Taifa, Rahma, naye alikuwepo ukumbini humo akipata raha kamili.
Mtangazaji wa Star Tv, Sauda Mwilima (kulia) akiwa na mwenzake wakifuatilia kwa makini.
Msanii AY, akitoa raha kamili jukwaani.
Waziri wa habari, Vijana Utamaduni na Michezo, Emmanuel Nchimbi (kushoto) akiwa na Katibu Mkuu wa Shirikisho la mpira wa miguu nchini TFF, Angetile Osiah.
Msanii wa maigizo, Monalisa, akiwa na Alirehmtula jukwaani, baada ya kukabidhi tuzo.
Rose Ndauka, akimkabidhi tuzo ya pili C-Pwaa, baada ya kuibuka katika Kategoli ya Video bora mwaka.
Mtangazaji wa redio Times, akimkabidhi tuzo msanii Barnaba, baada ya kuibuka kidedea katika kategoli ya Wimbo bora wa Zouk Rhumba. katikati ni Mzee wa Planet Bongo, Dullah.
Msanii Linah, akiimba kwa hisia jukwaani.
Patricia Hirary, akimkabidhi tuzo, Mpoki baada ya kuibuka kidedea katika Kategoli ya Wimbo bora wa Asili na wimbo wake wa Shangazi.
Kipa wa Simba, Juma Kaseja (kushoto) akimkabidhi Tuzo Mzee Yusuph, baada ya kuibuka kidedea katika Kategoli ya Wimbo bora wa Taarab. Kulia ni beki wa Yanga, Shadrack Nsajigwa.
Mpoki akizungumza na kuwashukuru mashabiki wake baada ya kupokea tuzo hiyo.
Mapaparazi wa vyombo mbalimbali vya habari, wakiwa bize kupata picha za matukio jukwaani.
Msanii Diamond, akiimba jukwaani ikiwa ni sehemu ya burudani zilizoandaliwa usiku huo.
Waendesha shughuli Ma Mc, Millad Ayo na mwenzake wakiwajibika jukwaani.
Bi Kidude, akiwa ni miongoni mwa wasanii walioalikwa katika onyesho hilo.
Mgosi (katikati) na Tegete, wakipata menu ukumbini humo.
Wasanii wa kundi la Tanzania House of Talent THT, wakishambulia jukwaa.
MAFOTO PRODUCTION & ENTERTAINMENT KWA MAHITAJI YAKO YA STILL PICTURE, VIDEO SHOOTING, MUSIC & Mc's KATIKA SHEREHE YA AINA YEYOTE. VIDEO EDDITING, COVER DISGNING, PPS ZA DK 3, POSTERS ZA AINA MBALIMBALI COVER CD PRINTING, BURNING CD N.K. WASILIANA NASI KWA NO, 0787 200005/0754, 0655-306109/0714 656660 BARUA PEPE:- muhidinuk@yahoo.co.uk,sufianimafotoblog@gmail.com AMA TEMBELEA www.sufianimafoto.com
Samia aijaza Manoti Stars
-
RAIS Samia Suluhu Hassan ameiwazadia timu ya soka ya Taifa, ‘Taifa Stars’
Sh milioni 200 kuelekea mchezo wa robo fainali wa michuano ya Mabingwa wa
Af...
NBAA YAWANOA WATAHINIWA MITIHANI CPA
-
Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) imeendesha
warsha kwa njia ya mtandao pamoja na mafunzo ya ana kwa ana kwa wanafunzi
wan...
‘NINJA’ HIMID MAO MKAMI NAYE AREJEA AZAM FC
-
KLABU ya Azam FC imemtambulisha kiungo Himid Mao Mkami (32) kuwa mchezaji
wake mpya kwa mkataba wa mwaka mmoja hadi mwaka 2026 akitokea Ghazl El
Mahallay...
Habari kubwa Magazetini Kenya leo March 3, 2025
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania March 3, 2025,nakukaribisha
kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za nyuma Magazetini
ke...
-
[image: Tumore prostatico: la prognosi in base a stadio, grado e rischio]
Tumore prostatico: la prognosi in base a stadio, grado e rischio
alt=”” class=”w...
DIAMOND PLATINUMZ HOUSE 'STATE HOUSE'
-
Bila shaka muziki unalipa na ndio maana mwanamuziki wa Bongo Fleva, kutoka
Tanzania Naseeb Abdul 'Diamond Platnumz, ameweza kujenga nyumba jambo
ambal...
No comments:
Post a Comment