Habari za Punde

*TAIFA STARS YAWAPA RAHA WATANZANIA, YAIBUKA NA USHINDI WA 2-1

Mabeki wa timu ya Jamhuri ya Afrika ya Kati, wakijaribu kuokoa mpira uliowashinda na kutinga wavuni na kuandika bao la pili na la ushindi baada ya kupigwa na Mbwana Samatta kwa kichwa, wakati wa mchezo dhidi yao na Taifa Stars wa kuwania kufuzu kucheza kuwania kufuzu kucheza fainali za Mataifa ya Afrika zitakazofanyika nchini Gabon na Equatorial ya Guine mwaka 2012. Taifa Stars imeshinda 2-1.
Wachezaji wa Taifa Stars, wakishangilia bao la pili lililofungwa na Mbwana Samatta, kipindi cha pili.
"Oooh, Yeeees!
Kocha Mkuu wa taifa Stars, Jan Poulsen, akishangilia bao la ushindi lililofungwa na Mbwana Samatta.
Mashabiki wa Soka wa Taifa Stars, wakishangilia baada ya timu yao kuibuka na ushindi.
Baadhi ya Viongozi wa timu ya Jamhuri ya Afrika ya Kati, wakimzonga Kamisaa wa mchezo baada ya kumalizika kwa mchezo huo, wakidai hakuongeza dakika za nyongeza.
Mashabiki wakiwa na huzuni, wakati mchezo ukiendelea na Taifa Stars ikiwa nyuma kwa bao 1-0.
Juma Kaseja na Mussa Mgosi, wakiwa jukwaani wakifuatilia mchezo huo.
Kiungo wa Taifa Stars, Henry Joseph (katikati) akiwatoka mabeki wa timu ya Jamhuri ya kati.
Mohamed Banka, akimiliki mpira mbele ya beki wa timu pinzani, wakati wa mchezo huo.
Kipa wa timu ya Jamhuri ya Afrika ya Kati, akiruka kuokoa moja ya hatari zilizoelekezwalangoni kwake.













No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.