Habari za Punde

*BAADA YA SERIKALI KUFUNGA BAADHI YA NJIA WANANCHI WATUMIA HELIKOPTA KUTUA LOLIONDO KWA BABU

Helikopta ikitua katika uwanja ulio jirani na nyumbani kwa Mchungaji Ambilikile Masapile, kijijini Samunge, jana. Mfanyabiashara Hans Macha, alikodi Helikopta hiyo kwa ajili ya kuipeleka familia yake, akiwamo mama yake mzazi.

Baadhi ya wananchi wakipata huduma ya kununua mahitaji kutoka katika basi lililogeuka duka na kutoa huduma hiyo kijijini hapo. Hali kama hii ya basi kugeuzwa duka ni kawaida kabisa katika Kijiji
cha Samunge, Loliondo kwa Mchungaji Mstaafu Ambilikile Masapile., bidhaa hizo ni maalumu kwa ajili ya kuwauzia waliomo kwenye basi hilo kuelekea Loliondo na wananchi wengine.

Dawa hii haichagui rangi, dini Kabila wala Uraia. Watu wa rangi, kabila na dini mbalimbali wanaendelea kumiminika nyumbani kwa Mchungaji Mstaafu Ambilikile Masapile kwa ajili ya kupata dawa kama wanavyoonekan a katika picha hii.




No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.