Habari za Punde

*UFUNGUZI WA KIKAO CHA KAMATI KUU YA CCM MJINI DODOMA LEO

Mwenyekiti wa CCM taifa, Jakaya Kikwete, Makamu Mwenyekiti CCM Zanzibar, Aman Abeid Karume (wa tatu kushoto), Rais wa Zanzibar, Dkt Ali Mohamed Shein na Mwenyekiti wa CCM Mstaafu, Ali Hassan Mwinyi (kushoto), Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara, Pius Msekwa (kulia) na Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Willson Mukama, wakiwa katika ufunguzi wa Kikao cha Kamati kuu kilichofunguliwa leo, katika Ukumbi wa CCM Makao Makuu mjini Dodoma.
Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete, akiingia katika Ukumbi wa CCM Makao Makuu mjini Dodoma, leo Julai 31, wakati wa ufunguzi wa Kikao cha Kamati kuu. Kulia ni Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Willson Mukama.
 Wajumbe, Abdulrahman Kinana Mjumbe wa Kamati Kuu, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano) Samia Hassan Suluhu (katikati) na Nape Nnauye, wakiwa ukumbini humo.
 Wajumbe, Waziri wa Ulinzi, Hussein Mwinyi (katikati) Stephen Wasila (kulia) na Waziri wa Mawasiliano Sayansi na Teknolojia, Profesa Makame Mnyaa Mbarawa.
Wajumbe, Waziri wa Mambo ya Ndani Shamsi Vuai Nahodha na Spika wa Bunge, Anne Makinda, wakiwa ukumbini humo.

No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.