Habari za Punde

*CARNIVAL KUBWA KULIKO ZOTE KATIKA MABALA YA ULAYA ILIVYOFANA

Msafara wa maandamano ukizunguka katika kitongoji cha Notting hill.
URBAN PULSE CREATIVE wakishirikiana na Miss Jestina Blog wanatujuza matukio katika picha ya 'Notting hill Carnival'  iliyofanyika Jumapili tarehe 28 agosti 2011. Hii ilikuwa siku ya kwanza Carnival ya watoto ambayo hufanyika kila mwaka tangu mwaka 1964 ambayo siku ya pili inafuatiwa na siku ya watu wazima. 

Maelfu ya watu zaidi walijitokeza katika mitaa ya Notting hill wakati wa Carnival hiyo ambayo ni tofauti na miaka yote pia iliyokuwa na usalama wa polisi 1000 wa ziada na kufanya Jumla ya polisi kufikia 6500, kwa ajili ya usalama na kufanikisha shuguli nzima ya wanachi walio hudhuria. 

Hii inatoka na maasi yaliyo tokea hivi karibuni katika kitongoji cha Tottenham na sehemu nyingine nchini Uingereza. 
Jumla ya watu 53 wanashikiliwa na polisi kutokana kutaka kufanya fujo katika carnival hiyo.

Msanii pekee katika tamasha hilo, Mish, akitoa burudani kutoka Urban Pulse na kufanya makamuzi ya ukweli.
Mremboa burudani jukwaani...
Mdau akipozi na vazi rasmi la Karnival hiyo.
Washkaji wakipata menu wakiwa katikamavazi yao ymaalum kwa Carnival hiyo baada ya misele mingi ya kuzunguka katika mitaa.
Raia wengine walishindwa kujumuika katika maandamnao hayo lakini walibaki katika majumba yao wakishuhudia kupitia madirishani.
Page Kutoka X Factor aliyekuja kutoa kampani kwa Mish wakati wa show.
Page kutoka X Factor, akipozi kwa picha na wadau.
Wadau wakila pozi na Jestina.




No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.