| | |
Pambano la mchujo kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika zitakazofanyika mwakani nchini Equatorial Guinea na Gabon kati ya Tanzania (Taifa Stars) na Algeria (Desert Warriors) limeingiza sh.148,220,000. Mechi hiyo ilichezwa Septemba 3 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Mashabiki waliokata tiketi kushuhudia pambano hilo ni 29,892. Viti vya kijani ambavyo kiingilio kilikuwa sh. 3,000 ikiwa viti hivyo ndivyo vilivyowavutia zaidi mashabiki wengi ambapo 17,650 ikiwa ni zaidi ya nusu ya mashabiki wote walionunua tiketi kwa ajili ya viti hivyo. VIP A ndipo kulikokuwa na kiingilio cha juu cha sh. 30,000, jumla ya mashabiki 394 walinunua tiketi kwa ajili ya eneo hilo. Viti vya bluu kiingilio kilikuwa sh. 5,000, mashabiki walionunua tiketi walikuwa ni 8,166. Viingilio vingine katika pambano hilo vilikuwa sh. 7,000 viti vya rangi ya chungwa, sh. 10,000 VIP C na sh. 20,000 VIP B. Boniface Wambura Ofisa Habari Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) | |
| | |
| | |
Rais Samia Akutana na Mkurugenzi wa Miradi Benki ya Dunia Afrika
-
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa
kwenye mazungumzo na aliyekuwa Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia
anayesimamia...
15 hours ago

No comments:
Post a Comment