Habari za Punde

*MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AHUDHURIA SHUGHULI ZA MAZIKO 'DUA' YA BALOZI MHINA

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiweka saini katika kitabu cha maombolezo wakati alipofika nyumbani kwa  aliyekuwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi CCM Taifa, marehemu Balozi Athuman Mhina, kwa ajili ya kuhudhuria shughuli za maziko, Madale jijini Dar es Salaam, leo.
 Makamu Wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na Mwenyekiti wa Wazazi wa CCM Zanzibar, Bi. Dogo Mabruk, wakati alipokuwa akiwasili nyumbani kwa aliyekuwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi CCM Taifa, marehemu Balozi Athuman Mhina, kwa ajili ya kuhudhuria shughuli za maziko, Madale jijini Dar es Salaam, leo Januari 3, 2012. Kulia ni Sophia Simba.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara, Pius Msekwa.
 Ridhiwani Kikwete (wa tatu kushoto) na Vita Kawawa (wa kwanza kulia) wakiwa na baadhi ya waombolezaji.
 Baadhi ya waombolezaji.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akijumuika na baadhi ya Viongozi na wananchi kuomba dua maalum kwa  aliyekuwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi CCM Taifa, marehemu Balozi Athuman Mhina, wakati wa shughuli za maziko zilizofanyika nyumbani kwa marehemu Madale jijini Dar es Salaam leo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na Mufti Mkuu wa Baraza la waislam Tanzania, Sheikh Shaaban Simba, wakati akiondoka nyumbani kwa aliyekuwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi CCM Taifa, marehemu Balozi Athuman Mhina.

No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.