Habari za Punde

*BREAKING NEEEEEWZ! GODBLESS LEMA 'OUT' ATEMESHWA UBUNGE WA JIMBO LA ARUSHA MJINI


MAHAKAMA Kuu Kanda ya Arusha leo imetangaza rasmi kumvua Ubunge aliyekuwa Mbunge wa jimbo la Arusha mjini,  Godbless Lema kwa tiketi ya CHADEMA.
Hukumu ya kesi hiyo iliyokuwa ikimkabili Lema kufuatia kutoa maneno machafu ya kumdhalilisha mpinzani wake kupitia CCM, Dkt. Batilda Burian, ambaye kwa sasa ni Balozi ya Tanzania nchini Kenya, imetolewa na Jaji Mfawidhi wa Kanda ya Sumbawanga, Gabriel Rwakibarila katika hukumu ya kesi yhiyo a kupinga matokeo ya Ubunge Jimbo la Arusha hilo yaliyo wasilishwa na wanachama watatu wa CCM waliotaka Mahakama Kuu Kanda ya Arusha kutengua ushindi wa Mbunge huyo.
Wana CCM hao waliofungua kesi hiyo ni pamoja na Mussa Mkanga (55), Happy Kivuyo (49) na Agnes Molle (44).
Kuvuliwa Ubunge kwa Lema, kutatonesha na kuzima furaha za Chama chake ambacho bado  kipo katika shamra shamra za ushindi wa Ubunge jimbo la Arumeru Mashariki mkoani humo.
Pia habari za ndani ya Chama cha Chadema zinasema kuwa tayari Chama hicho kilisha soma alama za nyakati mapema katika kesi hiyo miezi kadhaa nyuma na kujipanga endapo mbunge huyo atavuliwa wadhifa wake nani atasimamishwa kutetea kiti hicho.
Habari hizo zinadai kuwa Chadema kimepanga kumsimamisha Katibu Mkuu wa Chama hicho na Mgombea Urais wa 2010, Dk. Wilbroad Silaa kutetea kiti hicho.
Aidha Wanachama hao wanadai kuwa taratibu za maadili ya uchaguzi zilikiukwa  kuwa mshindi alitumia lugha za kashfa, matusi na kejeli katika mikutano ya kampeni aliyofanya jimboni Arusha.
Katika kesi hiyo wadai walileta mashahidi 14 kwenda kutoa ushahidi wao katika mahakama hiyo na wadaiwa walifanikiwa kuwaleta mashahidi 5 kujitetea.

 

No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.