Mshambuliaji wa timu ya Taifa 'Taifa Stars' Mrisho Ngasa (kushoto) akichuana kuwania mpira na beki wa Ivory Coast katika mchezo wa kuwania tiketi ya kufuzu kutinga katika fainali ya kombe la dunia 2014, mchezo uliochezwa jana usiku. Katika mchezo huo Mshambuliaji wa Chelsea Solomon Kalou, ndiye aliyeanza kuibomoa ngome ya Stars kwa kufunga bao la kwanza katika dakika ya 23 ya kipindi cha kwanza, na msumali wa pili na mwisho ukipigiliwa na mshambuliaji pia wa Chelsea ya Uingereza Didie Drogbana. Kwa matokeo hayo sasa Stars inatakiwa ushindi wa zaidi ya magoli matatu kwa bila katika mchezo wake wa marudiano utakaochezwa hapa nyumbani katika uwanja wa Taifa.
KAMPUNI YA RADDY ENERGY YA TANZANIA KUNUNUA MITAMBO YA UZALISHAJI UMEME
KUTOKA KAMPUNI YA SIEMENS YA USWIDI
-
*Balozi wa Tanzania nchini Uswidi, Mhe. Mobhare Matinyi (wa nne kutoka
kushoto mstari wa mbele), akiwa pamoja na Mkurugenzi Mwendeshaji wa Raddy
Energ...
1 hour ago
No comments:
Post a Comment