Kocha mpya wa Klabu ya Yanga, Mbelgiji Thom Saintfiet, akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere, Dar es Salaam jana na kupokelewa mashabiki wa Klabu hiyo. Kocha huyo baada ya kuwasili anatarajia kusaini mkataba ramsi na Klabu hiyo, leo ambapo atakabidhiwa mikoba ya kujenga kikosi cha Yanga na kusimamia kikosi cha timu ya Vijana wa U 20 wa timu hiyo. Kocha huyo tayari amekwisha toa matumaini makubwa kwa wapenzi wa Klabu hiyo na wachezaji huku akisema kuwa kazi kubwa na ya kwanza ataanza kuandaa kikosi cha kutetea Ubingwa wa Kombe la Kagame katika michuano inayotarajia kuanza hivi karibuni.
NBAA YAENDELEA KUTOA ELIMU YA TAALUMA YA UHASIBU KWA WANAFUNZI WA CHUO
KIKUU CHA MZUMBE
-
Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) imeendelea
kutoa elimu na mafunzo kwa vyuo vikuu pamoja na shule za sekondari ikiwa na ...
7 hours ago

No comments:
Post a Comment