Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Bw. Zelothe Stephen.
Na. Luppy Kung’alo wa Jeshi la Polisi Dodoma
Abiria wanne waliokuwa wakisafiri katika Daladala (Hiace) iliyokuwa inatokea Dodoma kuelekea kijiji cha Mkanda wilayani Manyoni Mkoa Singida wamepoteza Maisha katika tukio la ajali na kuwaacha abiria wengine kumi na nane wakiwa majeruhi.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Bw. Zelothe Stephen alithibitisha kutokea kwa ajali hiyo akieleza kuwa ilitokea siku ya Jumapili tarehe 14/10/2012 majira ya saa kumi jioni (16:00hrs) katika Kijiji cha Uhelela Kata ya Bahi Wilaya ya Bahi Mkoa wa Dodoma katika barabara kuu ya Dodoma/Singida.
Bw. Zelothe Stephen alisema ajali hiyo ilihusisha gari lenye namba za usajili T.518 AVQ aina ya SCANIA likiwa na tela lenye namba za usajili T.780 AVK lililokuwa linaendeshwa na Dereva TUTU ACKSON mwenye umri wa miaka 23, Mkazi wa Chaduru, na gari namba T. 803 AHX aina ya TOYOTA HIACE lililokuwa likiendeshwa na DANIEL JACKSON mwenye umri wa miaka 46, mkazi wa Dodoma.
Aliwataja waliopoteza Maisha katika ajali hiyo kuwa ni abiria wanne waliokuwa wakisafiri na Hiace hiyo ambao ni MASHAKA ELIA mwenye umri wa miaka (27) ambaye ni kondakta, mkazi wa Chang’ombe Mkoani Dodoma, MOSI MAUNDAA mwenye umri wa miaka (55) mkazi wa wilaya ya manyoni, EZEKIELI MASALITO mwenye umri wa miaka kati ya (40-45) mkazi wa Makanda wilaya ya Manyoni na DASTAN KIPINGU mwenye umri wa miaka (35) ambaye hakufahamika ni mkazi wa wapi.
Mkuu huyo wa Polisi Mkoa wa Dododma alisema Miili ya marehemu hao imehifadhiwa katika Kituo cha Afya cha Wilaya ya Bahi ikisubiri kuletwa katika Hospitali ya Mkoa wa Dodoma kwa Uchunguzi zaidi wa Daktari, wakati majeruhi wengine kumi na tano (15) wamelazwa katika Hospitali ya Mkoa wa Dodoma kwa matibabu zaidi.
“Katika ajali hiyo Abiria kumi na nane (18) walijeruhiwa akiwemo Dereva wa Daladala hiyo, ambapo kati yao wanaume waliojeruhiwa ni 15 akiwemo mtoto mdogo mmoja na wanawake watatu (3).” Alifafanua Kamanda Zelothe
Bw. Zelothe aliwataja waliotibiwa na kuruhusiwa kuwa ni ESTER FUNGA mwenye umri wa miaka (30) mkazi wa Kintinku wilayani Manyoni, aliyejeruhiwa katika mkono wa kushoto na usoni, CHRISTINA DANIEL mwenye umri wa miaka (25) mhudumu wa hoteli, mkazi wa Ipagala, ambaye ameumia mkono wa kulia na mguu wa kulia na GREYSON OMARY mwenye umri wa mwaka mmoja na nusu, mkazi wa Kintinku wilayani Manyoni ambaye ameumia kichwani.
Aidha Kamanda Zelothe alitaja orodha ya majina ya waliojeruhiwa kuwa ni
DANIEL JACKSON @ NZOYA mwenye umri wa miaka (46) Dereva wa Toyota Hiace, mkazi wa Bahi road Dodoma, ANTONY CHAKA mwenye umri wa miaka (23) mkazi wa Makanda Manyoni, JOSEPH CHRISOPHER mwenye umri wa miaka (40) mkazi wa Makanda, VENANCE MIRAJI mwenye umri wa miaka (40) mkazi wa Kintinku wilayani Manyoni, MASONGA BURUGE mwenye umri wa miaka (40) mkazi wa Kintinku wilayani Manyoni, PROTAS MWALUKO mwenye umri wa miaka (70) mkazi wa Makanda wilayani Manyoni na PEASON MAGUMILA mwenye umri wa miaka (30) mkazi wa Kibaigwa wilayani Kongwa.
Wengine ni TIMITA MADATILO mwenye umri wa miaka (30) mkazi wa Makanda wilayani Manyoni, MATONYA MWENDAUHEMBA mwenye umri wa miaka (40) mkazi wa wilaya ya Bahi, MASHAKA ELIA mwenye umri wa miaka (27) mkazi wa Chang’ombe Dodoma, TITUS MTWEVE mwenye umri wa miaka (32) mwalimu wa shule ya sekondari Manyoni, JUMA SHABANI mwenye umri wa miaka (35) mkazi wa Makanda wilyani Manyoni, SOPHIA LEMA mwenye umri wa miaka (52) mkazi wa Kintinku wilayani Manyoni, RAMADHANI ABDALLAH mwenye umri wa miaka (38) mkazi wa wilyani Manyoni na mwanaume ambaye hajafahamika jina mwenye umri kati ya (35-40) ambaye hali yake ni mbaya.
Bw. Zelothe Stephen alisema uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa chanzo cha ajali hiyo ni uzembe wa dereva wa lori hilo ambaye aliigonga kwa nyuma gari hilo la abiria iliyokuwa mbele yake na kuitoa nje ya barabara na kusababisha ajali hiyo, Dereva wa Lori hilo lililokuwa linatoka Dar es Salaam likielekea Kigoma amekamatwa na utaratibu wa kumfikisha mahakamani unaandaliwa.
Imetolewa na
POLISI MKOA WA DODOMA
DAWATI LA HABARI, ELIMU NA MAHUSIANO,
CONTACT:
Phone: 0715 006523, Luppy Kung’alo – Mrakibu msaidizi wa Polisi (ASP)
Phone: 0712 360203, Silyvester Onesmo – Police Konstebo (PC)
|
*WANNE WAPOTEZA MAISHA KATIKA AJALI (W) BAHI-DODOMA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
MATANGAZO MADOGO MADOGO

MAFOTO PRODUCTION & ENTERTAINMENT KWA MAHITAJI YAKO YA STILL PICTURE, VIDEO SHOOTING, MUSIC & Mc's KATIKA SHEREHE YA AINA YEYOTE. VIDEO EDDITING, COVER DISGNING, PPS ZA DK 3, POSTERS ZA AINA MBALIMBALI COVER CD PRINTING, BURNING CD N.K. WASILIANA NASI KWA NO, 0787 200005/0754, 0655-306109/0714 656660 BARUA PEPE:- muhidinuk@yahoo.co.uk,sufianimafotoblog@gmail.com AMA TEMBELEA www.sufianimafoto.com
BLOGU RAFIKI
-
-
JESHI la Polisi Mkoa wa Morogoro limewakamata watuhumiwa wanne wakiwa na jumla ya vipande 23 vya meno - JESHI la Polisi Mkoa wa Morogoro limewakamata watuhumiwa wanne wakiwa na jumla ya vipande 23 vya meno ya Tembo, katika operesheni iliyoshirikisha askari ...6 hours ago
-
Mgombea Ubunge wa Viti Maalum Pwani Aongoza Wanawake Kumkaribisha Dkt. Samia Mkuranga - Mgombea Ubunge wa Viti Maalum Mkoa wa Pwani kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mariam Ibrahim, ameongoza maandamano ya wanawake wa Mkoa wa Pwani kwa ajil...7 hours ago
-
NEWALA WAIPA KONGOLE REA MRADI WA KUSAMBAZA UMEME VITONGOJINI - -Waeleza kuridhishwa na kasi ya utekelezaji wake -Wasema umeibua fursa lukuki Wakazi wa vitongoji vya Chihanga, Mpilipili, Mkwedu na Majengo Wilayani Newa...9 hours ago
-
Elimu : Bajeti za Elimu Zisipuuzwe wakati wa misukosuko ya Kiuchumi na Kisiasa Duniani - Kikwete na Malala Waonya. - Rais Mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete na mshindi wa Tuzo ya Amani ya Nobel, Malala Yousafzai, wameonya juu ya mwenendo hatarishi duniani wa kupunguza au ku...2 days ago
-
UNESCO Yaunga Mkono Juhudi za Serikali Kuboresha Mfumo wa Usimamizi wa Mafunzo Endelevu ya Walimu (MEWAKA) - [image: Picture1] [image: Picture2] [image: Picture3] [image: Picture4] [image: Picture5] Na Mwandishi Wetu, Arusha. Wizara ya Elimu, Sayansi na Tekno...5 weeks ago
-
Ecobank yasherehekea miaka 40 kwa kampeni ya “Gutuka na Ecobank” - Meneja Mwandamizi wa Kitengo cha Wateja Binafsi Ecobank Tanzania, Innocent Urio (wa pili kulia) akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kampeni maalum ...5 weeks ago
-
TAIFA STARS YACHAPWA 1-0 NA NIGER ZANZIBAR KUFUZU KOMBE LA DUNIA - TIMU ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars jana ilichapwa bao 1-0 na Niger pungufu katika mchezo wa Kundi E kufuzu Fainali za Kombe la Dunia 2026 Uwanj...5 weeks ago
-
Habari kubwa Magazetini Kenya leo March 3, 2025 - Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania March 3, 2025,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za nyuma Magazetini ke...7 months ago
-
-
BODI YA MAJI BONDE LA KATI YAWATAKA WANANCHI KUCHUKUA TAHADHARI KUFUATIA MAFURIKO KWENYE MAZIWA YA KINDAI, MUNANG NA SINGIDANI - * Mhandisi Rasilimali za Maji, Bodi ya Maji Bonde la Kati, Moses Salumbi (kushoto), akiweka alama za ukomo wa maji ya mafuriko kwenye Maziwa ya Kindai na...5 years ago
-
MSANII DIAMOND AZINDUA WIMBO WA COLOURS KWA AJILI YA KOMBE LA DUNIA 2018 NCHINI URUSI - Cathbert Kajuna To:amichuzi,othmanmichuzi,MUHIDIN MICHUZI,Geofrey Adroph Bcc:fungoomar@yahoo.com May 15 at 6:00 AM Msanii Diamond akipagawisha mashabiki wa...7 years ago
-
RAIS JOHN MAGUFULI AKUTANA NA RAIS WA JCA NA BALOZI WA JAPAN IKULU JIJINI DAR ES SALAAM - *Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia jambo na Rais wa shirika la Kimataifa la Maendeleo la Japan (JICA) Bw. Shini...8 years ago
-
JOSE MOURINHO HAS REPORTEDLY 'SHOKED' SOME OF HIS MANCHESTER UNITED PLAYERS - *Jose Mourinho might have hoped for a longer honeymoon at Manchester United, but three defeats in a row, in the space of a week, have led to the first maj...9 years ago
-
TIBA YA MAGONJWA YAKO NA MATATIZO MBALIMBALI SASA HII HAPA BEI NAFUU SOMA HAPA KWA MAKINI - Je? Unaumwa au unasumbuliwa na matatizo yoyote kiafya? Unahitaji msaada wa haraka, tuna virutubisho sahihi kuondoa magonjwa kama kisukari, presha, uvimb...9 years ago
-
DIAMOND PLATINUMZ HOUSE 'STATE HOUSE' - Bila shaka muziki unalipa na ndio maana mwanamuziki wa Bongo Fleva, kutoka Tanzania Naseeb Abdul 'Diamond Platnumz, ameweza kujenga nyumba jambo ambal...10 years ago
-
SIMBA ILIPOWASHANGAZA MASHABIKI WA SOKA JANA,ILIPOCHOMOA MABAO 3 NA KULAZIMISHA SARE YA 3-3 - * Beki wa Yanga, Nadir Haroub 'Canavaro', akiwania mpira na kipa wa Simba Abel Dhaira, wakati wa kipindi cha pili cha mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanza...11 years ago
-
-
-
-
No comments:
Post a Comment