Mchezo
 wa Ligi Kuu ya Vodacom kuwania ubingwa wa Tanzania Bara kati ya Yanga 
na Ruvu Shooting uliopangwa kuchezwa kesho (Oktoba 20 mwaka huu) Uwanja 
wa Chamazi sasa umehamishiwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 
10.15 jioni.
Mabadiliko
 hayo yamefanyika kutokana na maombi ya timu hizo mbili kutaka mechi 
ichezwe Uwanja wa Taifa kutokana na sababu mbalimbali ambazo zimeridhiwa
 na Kamati ya Ligi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) 
ikiwemo siku hiyo uwanja huo kutokuwa na mechi.
Viingilio
 katika mechi hiyo itakayokuwa chini ya mwamuzi Amon Paul kutoka Mara ni
 sh. 5,000 viti vya kijani na bluu, sh. 8,000 viti vya rangi ya chungwa,
 sh. 15,000 VIP B na C na sh. 20,000 kwa VIP A.
 Pia
 Kamati ya Ligi imekataa ombi la timu ya Azam kutaka mechi zake za 
nyumbani za ligi hiyo zichezwe dhidi ya Simba na Yanga zichezwe Uwanja 
wa Chamazi kutokana na sababu za kiusalama.
Pia
 Kamati ya Ligi imekataa ombi la timu ya Azam kutaka mechi zake za 
nyumbani za ligi hiyo zichezwe dhidi ya Simba na Yanga zichezwe Uwanja 
wa Chamazi kutokana na sababu za kiusalama.
Nayo
 Coastal Union itakuwa mwenyeji wa Mtibwa Sugar katika mechi nyingine ya
 ligi hiyo itakayochezwa kesho (Oktoba 20 mwaka huu) katika Uwanja wa 
Mkwakwani jijini Tanga.
Mchezo
 huo namba 56 wa kukamilisha raundi ya nane utachezeshwa na mwamuzi 
Israel Nkongo atakayesaidiwa na Hamis Chang’walu na Omari Kambangwa, 
wote kutoka Dar es Salaam.
Ligi
 hiyo itaendelea tena Jumapili (Oktoba 21 mwaka huu) kwa mechi tatu. JKT
 Ruvu itaoneshana kazi na Oljoro JKT kwenye Uwanja wa Chamazi, Mgambo 
Shooting itaikaribisha Simba kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga 
wakati Tanzania Prisons na Toto Africans zitapimana ubavu kwenye Uwanja 
wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya.

 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment