Habari za Punde

*BENKI YA BARCLAYS TANZANIA YASHINDA TUZO BENKI BORA YA MWAKA 2012 NCHINI


BENKI ya Barclays Tanzania (BBT) imetangazwa kuwa mshindi wa Tuzo ya Benki Bora kwa mwaka 2012 hapa Tanzania. Taarifa hiyo ilitolewa jijini London, Uingereza, Alhamisi ya Novemba 29 mwaka huu wakati wa hafla ya Tuzo za Benki ya Mwaka zinazoratibiwa na kusimamiwa na gazeti la Financial Times.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Mkurugenzi Mtendaji wa BBT, Bwana Kihara Maina alisema: “Lengo letu ifikapo mwaka 2015 ni kuhakikisha kila mtu anataka kuja kwetu kwa kupitia kauli mbiu ya ‘Kaweke Pesa Benki’ (Go-to-bank). Heshima hii kubwa kwetu imeletwa na moyo wa kujitoa wa wafanyakazi kwa kuwahudumia vyema wateja wetu na hivyo kuyarahisisha maisha yao.”

Bw.Maina aliongeza: “Kwa jumla Tanzania kuna benki 50 na kuchaguliwa kuwa Benki Bora nchini ni furaha kubwa kwa wanafamiliwa wa Barclays, wateja na wadau wote. Hii ni kwa kutambua uwekezaji wetu mkubwa tulioufanya katika biashara ili kutoa huduma bora kwa wateja wetu.

 Tunawaahidi Watanzania kuwa tutawekeza zaidi na kutoa huduma za kibenki zinazokubalika duniani.”

Kwa mujibu wa jarida lifahamikalo kama ‘The Banker Magazine’, Barclays imeshinda tuzo hiyo ya mwaka kutokana na matumizi ya Teknolojia ya Mawasiliano kama vile uwekezaji katika mfumo wa kazi (workflow and imaging systems), kuanzisha huduma za bure za ATM, kuanzisha huduma za kibenki kwa njia ya mtandao, maendeleo katika biashata ndogo ndogo na za kati (SMEs) na kuongezeka kwa faida mwaka 2010 na 2011.

Kwa maelezo zaidi wasiliana na:
Tunu Kavishe
Head of Corporate Affairs
Barclays Bank Tanzania
+255 228 2018
tunu.kavishe@barclays.com 

About Barclays
Barclays is a major global financial services provider engaged in personal banking, credit cards, corporate and investment banking, and wealth and investment management. With over 300 years of history and expertise in banking, Barclays operates in over 50 countries and employs approximately 140,000 people. Barclays moves, lends, invests and protects money for customers and clients worldwide. For more information, please visit the Barclays website: www.barclays.com 

About Barclays in Africa
The businesses in scope for the proposed combination employ more than 8,000 people and have a network of more than 400 branches and 750 ATMs serving approximately 2.2 million customers.  As at December 2011, the Barclays Africa businesses in scope for the proposed combination had total assets of approximately GBP6 billion.

About Barclays Tanzania
Barclays Bank Tanzania Limited first opened its doors in Tanzania in 1925 and continued to operate in the country until 1967 when its Tanzania operations were nationalized to become National Bank of Commerce. With the liberalization of the economy in 1990s, Barclays Bank Plc made a decision to re-enter the Tanzania market and re-opened its doors in the year 2000. Barclays Bank Tanzania now has 22 branches, 41 ATMs strategically located countrywide, over 400 employees and over 110,000 customers. 

                                          

No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.