Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akiwasalimia wananchi baada ya kuwasili eneo la Nane Nane mkoani Morogoro kuanza ziara ya siku nane ya kikazi mkoani humo, leo wakati wa mapokezi yake yaliyofanyika eneo la Nane Nane, nje kidogo ya mji wa Morogoro.
Baadhi ya waendesha pikipiki wakionekana kuwa na hamasa kubwa wakati wakisindikiza msafara wa Kinana kuingia mjini Morogoro leo.
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akijaribu moja ya pikipiki, kabla ya msafara wa Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana kuondoka eneo la Nane Nane kwenda Morogoro mjini kuanza ziara ya kikazi mkoani humo.
No comments:
Post a Comment