Habari za Punde

*MAOFISA WA JESHI LA RWANDA, GHANA WATEMBELEA TBL DAR

 Mpishi wa Bia wa kampuni hiyo, Kelvin Nkya, akiwapatia maelezo maofisa wa majeshi ya Rwanda na Ghana, kuhusu idara mbalimbali za uzalishaji walipotembelea kiwanda cha bia cha Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Dar es Salaam hivi karibuni. Maofisa hao waliongozwa na maofisa wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).

Meneja Uhusiano Mambo ya Nje wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Emma Oriyo akiwapatia maelezo ya awali maofisa hao wa kijeshi kutoka nchi hizo mbili.
 Maofisa wakiwa idara ya upishi wakipata maelezo ya jinsi bia inavyopikwa kisasa kwa kutumia kompyuta.
Kwa Picha zaidi Bofya HAPA
 Meneja Uhusiano Mambo ya Nje wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Emma Orio (kushoto) akisalimiana na maofisa wa jeshi la Rwanda na Ghana waliofika kutembelea utendaji wa kampuni hiyo, Dar es Salaam hivi karibuni.
 Mpishi wa Bia wa TBL, Kelvin Nkya akiwapatia maelezo maofisa hao namna bia inavyopikwa kwa kutumia kompyuta.
 Baadhi ya maofisa wakijaza majina yao kwenye kitabu cha wageni TBL
 Brigedia Jenerali  Jean Jacques Mupenzi kutoka Jeshi la Rwanda, akimkabidhi zawadi Meneja wa Kiwanda cha Bia cha TBL Dar es Salaam, Calvin Martine baada ya kutembelea kiwanda hicho.
 Baadhi ya maofisa wakitembelea kiwanda hicho, idara ya packaging
 Meneja wa Kiwanda cha TBL Dar es Salaam, Calvin Martine akimpatia zawadi Brigedia Jenerali  Jean Jacques Mupenzi kutoka Jeshi la Rwanda.
 Maofisa wakipata maelezo katika idara ya uchachuaji bia
Maofisa hao wakiwa katika picha ya pamoja na maofisa wa TBL baada ya kumalizika kwa ziara hiyo.

No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.