Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari , Vijana , Utamaduni na Michezo (WHVUM) Prof. Elisante Ole Gabriel (kulia) akizungumza na Bondia Mstaafu Rashid Matumla (Snake Man) alipomtembelea leo ofisini kwake jijini Dar es Salaam. Katika mazungumzo yao Prof Elisante alimtaka Bondia huyo kuandaa mipango na mikakati ya kuhakikisha anatafuta mrithi wake katika mchezo huo kwa kuwarithisha viajana watakaofuata nyayo zake na kufika mbali katika mchezo huo kimataifa. KUSOMA ZAIDI BOFYA READ MORE
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo ,Prof. Elisante Ole Gabriel (kulia) akiwa katika mazungumzo na Bondia Mstaafu ,Rashid Matumla leo jijini Dar es Salaam alipomtembelea ofisini kwake (wa pili kushoto) ni Mkurugenzi wa Michezo katika wizara hiyo, Leonard Thadeo (kushoto) no Ofisa Vijana katika wizara hiyo, Amina Sanga.
Picha ya pamoja - Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Prof. Elisante Ole Gabriel (mwenye miwani) Mkurugenzi wa Michezo katika wizara hiyo Leonard Thadeo( mwenye koti jeusi kulia), Bondia Mstaafu Rashid Matumla (mwenye fulana ya mistari)), pamoja na Afisa Vijana katika wizara , Amina Sanga(kushoto). Picha zote na Mwanakombo Jumaa- MAELEZO
*************************************************
*Serikali
yamtaka Matumla kurithisha kipaji chake kwa vijana
Na
Concilia Niyibitanga, Wizara
ya Hbari, Vijana, Utamaduni na Michezo
Serikali
kupitia Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo imemtaka Bw. Rashid Matumla
ambaye ni bondia mstaafu katika mchezo wa ngumi za ridhaa kurithisha kipaji
chake kwa vijana wengine.
Hayo
yamesemwa leo Jijini Dar es salaam na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,
Vijana Utamaduni na Michezo, Prof Elisante Ole Gabriel wakati akiongea na Bw.
Matumla alipomtembelea ofisi kwake. Prof.
Gabriel amemtaka kuanzisha kikundi cha vijana ambacho ataweza kukifundisha
mchezo huo ili kipaji chake kisipotee ukizingatia kuwa Tanzania ina wachezaji
wachache katika mchezo huo.
“Ni
vema ukarithisha ujuzi wako katika mchezo wa ngumi kwa vijana chipukizi kwa
kuwafundisha na kuwashauri katika mchezo huo” Amesema Prof. Gabriel.
Amesema
kuwa Serikali inatambua mchango wake katika mchezo wa ngumi hapa nchini na
hivyo si vema akakaa na ujuzi wake ukizingatia kuwa yeye amestaafu katika
mchezo huo.
Aidha,
Prof. Gabriel ameongeza kuwa kwa kufanya hivo Matumla atawasaidia vijana
chipukizi kuwa Mabondia wazuri wa baade ikiwa ni pamoja na kujiajiri badala
ya kujihusisha na vitendo vibaya kama matumizi ya madawa ya kulevya n.k
Naye
Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo, Bw. Leonard Thadeo amesema kuwa kikundi
hicho kinaweza pia kikajihusisha na ujasiriamali kwa kuomba mikopo katika Mfuko
wa Maendeleo ya Vijana kwa kuwa wanamichezo pia wanatakiwa kujishughulisha na
ujasiriamali ili kujiongezea kipato.
Kwa
upande wake Bw. Matumla amesema kuwa amefurahi na amefarijika sana kuongea na
viongozi wa wizara inayosimamia michezo na vijana kwa kuwa wameonesha kutambua
mchango alioliletea Taifa hili katika mchezo huo. Matumla
amesema kuwa atafanya kila awezalo kuhakikisha kuwa anawarithisha mabondia
chipukizi na vijana wengine kipaji chake katika mchezo huo ili wawe mabondia bora
wa baadaye.
No comments:
Post a Comment