Habari za Punde

*RAIS JK, MAKAMU WAKE DKT. BILAL WAWAONGOZA WANANCHI KUAGA MWILI WA MAREHEMU KAPTENI KOMBA KARIMJEE DAR

 Rais Jakaya Kikwete na mkewe Mama Salma Kikwete, wakitoa heshima za mwisho mbele ya Jeneza lenye mwili wa marehemu Kapteni John Komba, wakati wa shughuli za kuaga mwili huo zilizofanyika kwenye Viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam, leo mchana. Baada ya shughuli hiyo ya kuaga mwili huo ulisafirishwa kuelekea Jiji cha Litui, Wilaya ya Mbinga Mkoa wa Ruvuma kwa maziko, yanayotarajia kufanyika kesho. Leo jioni katika Uwanja wa Majimaji mjini Songea pia kutakuwa na shughuli ya kuaga mwili huo ambapo wakazi wa Mkoa huo watapata fursa ya kutoa heshima zao za mwisho.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, wakeze Mama Zakhia Bilal na Mama Asha Bilal, wakitoa heshima zao za mwisho mbele ya jeneza lenye mwili wa marehemu, Kapteni John Komba, wakati wa shughuli za kuaga mwili huo zilizofanyika leo, kwenye Viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam. Baada ya shughuli hiyo mwili wa marehemu umesafirishwa kuelekea Kijiji cha Litui Wilayani Mbinga mkoa wa Ruvuma kwa maziko.
 Wanafamilia wakiwasili kwenye viwanja hivyo...
 Mke wa marehemu Kapteni Komba, Mama Salome Komba, akiwasili kwenye viwanja hivyo.
 Wapambe wa Bunge la Jamhuri, wakibeba Jeneza lenye mwili wa marehemu wakati likiwasili kwenye viwanja hivyo.
 Jeneza hilo likiwa katika viwanja hivyo.
 Baadhi ya viongozi waliohudhuria shughuli hiyo kwenye viwanja vya Karimjee.
 Baadhi ya viongozi waliohudhuria shughuli hiyo kwenye viwanja vya Karimjee.
 Baadhi ya viongozi waliohudhuria shughuli hiyo kwenye viwanja vya Karimjee.
 Mwakilishi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Mhe. Joshua Nassari, akizungumza kutoa salamu za rambirambi kwa niaba ya upinzani.
 Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana, akizungumza kutoa salamu za rambirambi kwa niaba ya CCM.
 Spika wa Bunge la Jamhuri, Mhe. Anne Makinda, akizungumza kwa niaba ya wabunge.
 Mwandishi wa habari wa Uhuru, Mariam, akionekana kubugujikwa na machozi wakati wasanii wakiimba jukwaani.
 Msanii Lubi akiimba wimbo maalumu jukwaani.
 Wasanii wa muziki wa dansi wakiimba wimbo maalum jukwaani.
 Wasanii wa Bongo Flava na Bongo Movie wakiimba wimbo maalum jukwaani.
 Makamu wa Rais, Dkt. Bilal, akiagana na Spika wa Bunge Mstaafu, Pius Msekwa wakati akiondoka kwenye viwanja hivyo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowassa, wakati walipokutana kwenye Viwanja vya Karimjee baada ya kuhudhuria shughuli za kuaga mwili wa marehemu Kapteni John Komba leo. Baada ya shughuli hiyo mwili wa marehemu umesafirishwa kuelekea Jijini cha Litui Wilayani Mbinga mkoa wa Ruvuma kwa maziko. 

No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.