Habari za Punde

*HAFLA YA SIKU YA ELIMU MKOA WA DAR ES SALAAM, YAFANYIKA WILAYA YA ILALA

 Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Raymond Mushi, akisoma hotuba yake kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mecky Sadick, wakati wa hafla ya Siku ya Elimu Mkoa wa dar es Salaam, iliyofanyika leo mchana kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee, ambapo alikabidhi zawadi kwa wanafunzi wa shule mbalimbali za jijini zilizofanya vizuri kimasomo.
 Afisa Elimu wa Mkoa,  Raymond  Mapunda, Akizungumza wakati akimkaribisha mgeni rasmi na wageni waalikwa katika hafla hiyo.
 Katibu Tawala wa Mkoa wa dar es salaam, Theresia Mmbando akizungumza kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi kuhutubia. 
 Baadhi ya Wanafunzi wa Shule mbalimbali za Msingi waliofanya Vizuri, wakitambulishwa.
 Baadhi ya Wanafunzi walioshiriki katika hafla hiyo ya Siku ya Elimu Mkoa wa Dar Es Salaam.
Kikundi Cha Ngoma kutoka Shule ya Msingi Maktaba kikitoa burudani wakati wa hafla hiyo.
Mkuu wa Wilaya ya Ilala Raymond Mushi, akimkabidhi Tuzo Mkurungezi Mkuu wa Shule ya Msingi Tusiime, Ambaye Shule yake  Ilishinda kwa kuwa Shule Bora Mkoa wa Dar es Salaam. Picha na Miraji Msala

No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.