Habari za Punde

*WATANZANIA WASHAURIWA KUTUMIA SUMAJKT KATIKA MIRADI

 Mkurugenzi Habari na Mahusiano wa JKT  Kapteni Javan Bwai  akitoa maelezo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) leo jijini Dar es Salaam kuhusu mafanikio ya SUMAJKT kupitia kampuni ya ujenzi ya NSCD katika kipindi cha miaka 10 ya awamu ya nne ambapo alisema miradi 18 ya ujenzi imekamilika na miradi 9 inaendelea kujengwa . Kulia ni Kaimu Msemaji Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Meja Josephat Musira na kushoto ni Mkurugenzi wa ufundi SUMAJKT Mhandisi Fredrick Kaaya.
 Baadhi ya waandishi wa habari wakiwasikiliza viongozi wa JKT walipotembelea   jengo la kitega uchumi cha Kanisa la KKKT  ‘’Msasani Tower’’ lililopo Msasani jijini Dar es Salaam ambalo limejengwa na kampuni ya ujenzi ya JKT (NSCD).
Koplo Mhandisi Lazaro Masanja kutoka Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa akitoa rai kwa wananchi  na Taasisi kutumia Shirika la Uzalishaji Mali la JKT (SUMAJKT) kwenye utekelezaji wa miradi mbalimbali kwa gharama nafuu. Nyuma ni  jengo la kitega uchumi cha Kanisa la KKKT  ‘’Msasani Tower’’ lililopo Msasani jijini Dar es Salaam ambalo limejengwa na kampuni ya ujenzi ya JKT (NSCD). Picha na Georgina Misama -MAELEZO

No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.