Habari za Punde

*WATU NANE WAFARIKI KWA RADI MKOANI KIGOMA

 Mwalimu Veronika Mtes wa shule ya msingi Kibirizi aliyepata mshtuko baada ya tukio la radi akiwa katika hospitali ya Mawenzi mkoa wa Kigoma akipatiwa matibabu.
Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya mkoa wa Kigoma,Maweni akiongeza na Waandishi wa habari juu ya tukio la radi lililotokea jana na kuuwa watu 8, mkoani Kigoma.
************************************************
Na Editha Karlo,Kigoma
WATU wanane wanafunzi sita na mwalimu wa shule ya msingi kibirizi na mkazi wa eneo la Bangwe mjini hapa wamefariki dunia baada ya kupigwa na radi huku wanafunzi wengine 15 wakijeruhiwa na radi hiyo mchana wa jana.
Mganga mfawidhi wa Hospitali ya Mkoa wa kigoma (maweni) Dkt Fadhili Kabaya,  alisema kuwa watu hao walifikwa na umauti kufuatia mvua kubwa zilizonyesha zikiambana na radi zilizoanza majira ya saa sita mchana.
Dkt Fadhili aliwataja waliofariki katika tukio hilo kuwa ni pamoja na mwalimu wa shule ya msingi Kibirizi, Elinaza Mbwambo (25) Forcus Ntahaba (45) mkazi wa eneo la Bangwe mjini hapa.

Aliwataja wanafunzi waliofariki ambao wote ni wa darasa la kwanza kuwa ni Yusuph Ntahoma (8) Hassan Ally (9) Fatuma Sley (7) Zamda Seif (8) Shukranmi Yohana (7) na Warupe Kapupa (10).

Aidha, alisema walipokea majeruhi 15 lakini kati yao 10, waliruhusiwa baada ya kupatiwa matibabu baada ya hali zao kuwa nzuri na watano wamelazwa wanaendelea na matibabu katika hospital ya Mkoa wa Kigoma.
Akisimulia tukio hilo mwalimu aliyekuwa anafundisha darasani Mwalimu Merina Sililo,  alisema kuwa akiwa darasani akiendelea kufundisha ghafla aliona wingu zito jeusi limetanda hali iliyompelekea kushindwa kuendelea kufundisha kutokana na giza nene.
''Manyunyu yalianza kidogo kidogo ikaja mvua kubwa na radi pamoja na miungurumo mikali iliyopelekea wanafunzi kuanguka hovyo darasani na kuzimia,  na mara niliona moto umetanda katika chumba kizima cha darasa na mimi nilianguka chini na kupoteza fahamu''alisema mwalimu huyo

Alisema alipozinduka alijikuta katika hospital ya Mkoa akipatiwa matibabu baada ya kufikishwa kwa msaada wa waalimu wenzake.

''Kwakweli ni mungu tu mwenyewe ndo ameninusuru kwani nilirushwa mara tatu na radi na watoto wote darasani walikuwa wananiangukia mimi wengine walikuwa wanakimbia hovyo nje''alisema Mwalimu huyo. (Muro)

No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.