Habari za Punde

*KOMBE LA CHALENJI KILIMANJARO YAPANGWA NA WENYEJI CECAFA

Ratiba ya michuano ya Kombe la Challenji kwa Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati (Cecafa Senior Challenger Cup) imetoka jana ambapo timu ya Tanzania Bara ‘Kilimanjaro Star’ imepangwa kundi moja na wenyeji Ethiopia.
Katika taarifa ya CECAFA iliyotolewa jana, Kilimanjaro Star imepangwa kundi A pamoja na wenyeji Ethiopia, Somali na waaalikwa wa michuano hiyo timu ya Taifa ya Zambia ‘Chipolopolo’.
Kundi B lina  Bingwa mtetezi timu ya Kenya, Uganda, Burundi na Djibouti, huku kundi C likiwa na timu za Rwanda, Sudan, Sudan Kusini na Zanzibar.
Michuano hiyo inatarajiwa kuanza kutimua vumbi Novemba 21 nchini Ethiopia katika mji wa Addis Ababa na kumalizika Disemba 6 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.